Heshima ni Msingi wa Maelewano Duniani

Alfreda George - Wisdom&Wellness Counselor (TEWWY)

Masimulizi ...

by Alfreda George (Wisdom&Wellness Counselor - TEWWY).

Kulikuwa na dada mmoja ambaye alikuwa akijiona kuwa maisha ameyashinda na kwamba hana shida yoyote hapa duniani. Kwa vile alijiona kuwa Yeye ni ‘matawi ya juu’hakuna sababu ya kupoteza muda wake kuongea ama kushiriki ana na watu wa hadhi za chini. Alijitenga na kukaa mbali na jamii inayomzunguka, hakutaka kuongea na yeyote. Hata watoto wake hakutaka wakaribiane ama kucheza na watoto wenzao.

Siku moja akiwa kazini mtungi wa gesi ulileta hitilafu, msichana wa kazi alishutuka na kuogopa sana. Badala ya kutoka nje na kukimbia na watoto aliingia nao chumbani na kujifungia. Moto ulianza kuwaka na kusambaa haraka sana. Majirani aliokuwa ana wadharau na kuwaona si lolote mbele yake, walipoona nyumba inaungua na pia waliposikia kelele za watoto wakilia mle ndani, waliikimbilia nyumba, wakabomoa dirisha la chumbani na kuwatoa wale watoto. Watu ambao alikuwa anawadharau ndio waliokuja kumsaidia. Sebule na vyumba vyote vilishika moto. Msichana wa kazi na watoto wa mwenye nyumba walitolewa na majirani wakasalimika adha hiyo ambayo ingepelekea umauti wao. Lakini hakuna kitu hata kimoja kilichotoka mle ndani, vyote viliungua kabisa na moto. Hasara ilikuwa kubwa sana.

Majirani waliokuwa wakidharauliwa na mama huyo ndio waliotoka kumsaidia kwenye hili tukio la moto. Pamoja na kumsaidia kwa moyo moja walisikika wakimsema vibaya sana. Wangekuwa na roho mbaya wasingeweza hata kuwasaidia watoto wake.

Mama mwenye roho mbaya aliporudi toka kazini aliona yaliyotokea na kusikitika sana. Alipata fundisho kubwa sana. Aligundua kuwa wale aliowaona ni wajinga ndio waliowaokoa watoto wake.

Hadithi hii inatufundisha kutowadharau watu, inatupasa kumheshimu kila mtu bila kuangalia hali zao. Tuache kuwadharau watu hata kama hali zao ni mbaya kiasi gani kwani watakusaidia wakati wa matatizo. Na siyo hivyo tu, kila
binadamu ana haki ya kupendwa, kuthaminiwa na kuheshimiwa. Kwa maana hiyo, inatulazimu tuwe na mahusiano mazuri na binadamu wenzetu kwani mwanadamu siyo kisiwa, anaishi na watu. Heshima ni kitu cha bure lakini kina thamani sana. Ni lazima tutunze na kuomyesha kwa kila awaye katika maisha yetu ya kila siku hapa duniani.

The Healing Hands Project

The Healing Hands project will economically empower people to achieve financial autonomy by building entrepreneurial skills and embedding skills transfer within the community - eliminating poverty as a driver of ill mental health. Funds raised from the jewelry will help sustain the implementation of accessible psychosocial interventions in underserved communities and promote the economic empowerment of the grandmothers who have been trained in and are implementing WHO's mental health Gap Action Program. Healing Hands provides interpersonal counseling, group talk therapy, and psychoeducation resources delivered through arts, where clients learn to handcraft traditional beaded jewelry as a marketable skill. Follow us @TEWWYWisdom @WisdomWellnessCollection to stay up-to-date.

#MentalHealth #Grandmother #Wisdom #Wellness #mhGAP #HealingHands #Art #Culture #Tanzania

Previous
Previous

Akufaaye Kwa Dhiki Ndiye Rafiki

Next
Next

Mstahimilivu Hula Mbivu