
Upandacho Ndicho Uvunacho.
Katika kijiji kimoja alikuwepo mfanya biashara mmoja aliyekuwa akiuza siagi. Mfanya biashara huyu alikuwa na mteja wake maalum mjini ambaye alikuwa na duka kubwa la vyakula. Hawa wawili walikuwa na makubaliano ya kubadilishana bidhaa. Makubaliano hayo yalikuwa hivi: siagi katika vifungashio vya kilo moja moja,kwa bidhaa za vyakula tofauti tofauti. Kwa maana hiyo, wafanya biashara hawa wawili walikuwa hawauziani bali wanabadilishana kufuatana na makubaliano yao.

Maneno Matupu Hayavunji Mfupa.
Maneno ni matamshi yaliyoandikwa ama yaliyotamkwa kutoka kwenye vinywa vya watu. Mathalani, maneno yanaposemwa juu yako ni budi ukayatafakari kwanza ili ujue yana maana gani. Endapo maneno hayo hayaleti madhara yoyote basi hayatakuwa na shida kwako, shida itakuwa pale tu mtu atakapokushikia silaha na akakudhuru.

Mcheza Kwao Hutunzwa.
Mcheza kwao ni mtu ambaye anajishughulisha sana na mambo yanayofanyika kwenye jumuiya yake. Kutunzwa ni kupewa tuzo/zawadi pale atakapofanikisha jambo. Kiubinadamu huwa ni jambo zuri kutambuliwa mchango wao pale mtu afanyapo vizuri, iwe ni kwenye jumuia, masomo, kilimo ama eneo la kazi. Hata katika familia, inatakiwa zawadi zitolewe kwa wana familia.

Damu Nzito Kuliko Maji!
Samaki ni kiumbe kinachoishi majini. Mara baada ya kuvuliwa, baadhi ya samaki hutakiwa kukunjwa kwa ajili ya kuhifadhiwa au kwa matumizi ya baadaye. Ili huo mchakato uende vizuri ni lazima samaki hao wakunjwe kulingana na mahitaji ya mlaji. Endapo samaki atakawizwa kukunjwa mara baada ya kuvuliwa, huharibika kiasi kwamba hataweza kukunijka tena.

Msuli Tembo Matokeo Sisimizi.
Tembo ni mnyama mkubwa kuliko wote waishio porini. Kwa upande mwingine, sisimizi ni mdudu mdogo sana kiasi kwamba usipoangalia kwa makini, unaweza usimuone kwa jinsi alivyo mdogo.

Adui Mwombee Njaa.
Adui ni mwanadamu ambaye hayupo katika upande wa mwanadamu mwenzake yaani asiyekuwa na upendo kwa mwenzie. Njaa ni hali ya kukosa chakula. Sote tunajua kuwa mahitaji muhimu kwa mwanadamu ni chakula, mavazi na mahali pa kuishi. Mavazi na mahali pa kuishi sio muhimu sana ukilinganisha na mahitaji ya chakula kwa sababu bila chakula mtu hawezi kuishi.

Nyakati Ngumu Zisifunue Madhaifu Yako!
Maisha ya mwanadamu yamegawanyika katika maeneo mbalimbali na tofauti. Kipindi cha mpito hakina budi kutokea kwa kila mtu. Hakuna ambaye anaweza kusema hajapitia nyakati ngumu katika maisha yake. Kuna nyakati nyingine unapitia magumu kwa ajili ya kukuvusha na kukupeleka mahali fulani.

Samaki Mkunje Angali Mbichi!
Samaki ni kiumbe kinachoishi majini. Mara baada ya kuvuliwa, baadhi ya samaki hutakiwa kukunjwa kwa ajili ya kuhifadhiwa au kwa matumizi ya baadaye. Ili huo mchakato uende vizuri ni lazima samaki hao wakunjwe kulingana na mahitaji ya mlaji. Endapo samaki atakawizwa kukunjwa mara baada ya kuvuliwa, huharibika kiasi kwamba hataweza kukunijka tena.

Asiyekubali Kushindwa, Si Mshindani!
Kwa kawaida kuna mashindano ya aina mbali mbali katika nyanja tofauti tofauti kulingana na mazingira ya sehemu husika.Mtu yeyote anapoingia kwenye mashindano yoyote yale hutegemea kushinda. Lakini inapotokea ameshindwa, hulalamika au kuona kuwa kaonewa. Anasahau kuwa katika mashindano kuna mshindi na mshindwa. Mara zote mshindi huwa ni mmoja tu.

Muosha Huoshwa!
Mwosha kwa uelewa wangu ni mtu anayetumika kumwosha maiti na kumuandaa kwa mazishi. Zoezi hili la uoshaji hufanywa zaidi na watu wenye imani ya Dini ya Kiislamu. Kazi ya kuosha maiti huwa ni ngumu kidogo ndio maana inafanywa na watu maalumu. Na mwosha huyo naye akifa huoshwa vile vile na mwosha mwingine. Hayo ndiyo maisha yetu sisi wanadamu.

Kuugua Siyo Kufa
Kuugua ni hali ya kuwa na ugonjwa, na mtu mwenye ugonjwa hujulikana kama mgonjwa. Mtu anayeugua au mgonjwa hupenda kupata tiba ili aweze kupona. Mara nyingi mgonjwa anapozidiwa, fikra zinazomuujia ni kuwa anaondoka, yaani anakufa.

Hewala Si Utumwa!
Hewala ni neno linalomaanisha "ndiyo" au "ni sawa". Hii ina maana ya kukubali na siyo kulazimishwa kama vile ifanyikavyo kwa watumwa. Mtu anaweza kukubali tu ili wafikie suluhu katika kutokukubaliana kwao au kufikia muafaka kuwa basi na yaishe ili amani tipatikane.

Panapofuka Moshi Pana Moto.
Moshi ni hali ya ukungu wa joto na harufu ya kuunguzwa kwa majani, miti na hata karatasi. Hali hii unaweza kuiona kwa macho pia unaweza kuihisi kupitia kwenye pua. Kwa mfano huwezi kuona moshi unafuka kutoka msituni bila kuwa na moto nyuma yake. Hivyo moto huwa ndiyo sababu ya moshi kufuka.

Inyeshe Tuone Panapovuja
Mvua ni baraka ambayo huwanufaisha watu wote. Mkulima ama mfugaji akinufaika na mvua, mazao yapatikanayo kutoka kwao yatawanufaisha watu wote.

Usiache Tawi Kabla Hujashika Tawi!
Matawi ni sehemu ya mti ambayo huchipua katika mti na ile sehemu inayoshika majani. Ni kawaida ya mtu ambaye anapanda au anashuka mtini kushika tawi, asipofanya hivyo anaweza kuanguka.

Bidii Ina Tabia Ya Kumtabulisha Mtu.
Watu wengi tunafanya mambo lakini hatuyafanyi kwa bidii, tunafanya ili mradi tu yafanyike. Unaenda kazini lakini huna bidii ya kwenda kazini, leo unaenda kesho hauendi. Kila siku unaenda ukiwa wa mwisho na unatoka ukiwa wa kwanza.

Unaweza Kusahau Maumivu Lakini Sio Tukio!
Unaweza ukawa na maumivu fulani kama ni ya ugonjwa au maumivu mengine ya maisha. Maumivu hayo yanaweza kuwa ni ya muda fulani au kipindi fulani tu lakini mwisho yakapata jawabu. Katika hali hiyo unaweza ukasahau tu pindi pale linapokuja kupata majibu. Hapo itakuwa sio rahisi tena kukumbuka kama kuna jambo lilikuwa limekutesa. Mfano mzuri ni pale unapokuwa unaumwa lakini ukipona inakuwa sio rahisi tena kukumbuka maumivu uliyokuwa ukipata.

Jifunze Kutangaza Mema Kwa Ajili Yako.
Mara zote unatakiwa kutangaza mema kwa ajili yako. Kila mara jiambie, mimi sio wa kushindwa kwa sababu sikuumbwa kushindwa.

Maji Yakimwagika Hayazoleki!
Maji huwa yana nguvu sana yakiwa kwenye njia yake. Pamoja na umuhimu mkubwa wa maji kwa viumbe hai, yakimwagika umuhimu wake unakuwa haupo tena maana huwezi kuyazoa na kuyatumia.

Usilie Mbele Ya Adui, Hata Kama Unahitaji Msaada Wake.
Kupata na kukosa ndio maisha ambayo kila binadamu anapitia kila iitwapo leo. Kusaidiana katika shida na raha ndio kiulimwengu. Hapo ndipo tunapoonyesha upendo wetu kati ya mtu na mtu.