Upandacho Ndicho Uvunacho.

Upandacho Ndicho Uvunacho.

Katika kijiji kimoja alikuwepo mfanya biashara mmoja aliyekuwa akiuza siagi. Mfanya biashara huyu alikuwa na mteja wake maalum mjini ambaye alikuwa na duka kubwa la vyakula. Hawa wawili walikuwa na makubaliano ya kubadilishana bidhaa. Makubaliano hayo yalikuwa hivi: siagi katika vifungashio vya kilo moja moja,kwa bidhaa za vyakula tofauti tofauti. Kwa maana hiyo, wafanya biashara hawa wawili walikuwa hawauziani bali wanabadilishana kufuatana na makubaliano yao.

Read More
Mcheza Kwao Hutunzwa.

Mcheza Kwao Hutunzwa.

Mcheza kwao ni mtu ambaye anajishughulisha sana na mambo yanayofanyika kwenye jumuiya yake. Kutunzwa ni kupewa tuzo/zawadi pale atakapofanikisha jambo. Kiubinadamu huwa ni jambo zuri kutambuliwa mchango wao pale mtu afanyapo vizuri, iwe ni kwenye jumuia, masomo, kilimo ama eneo la kazi. Hata katika familia, inatakiwa zawadi zitolewe kwa wana familia.

Read More
Damu Nzito Kuliko Maji!

Damu Nzito Kuliko Maji!

Samaki ni kiumbe kinachoishi majini. Mara baada ya kuvuliwa, baadhi ya samaki hutakiwa kukunjwa kwa ajili ya kuhifadhiwa au kwa matumizi ya baadaye. Ili huo mchakato uende vizuri ni lazima samaki hao wakunjwe kulingana na mahitaji ya mlaji. Endapo samaki atakawizwa kukunjwa mara baada ya kuvuliwa, huharibika kiasi kwamba hataweza kukunijka tena.

Read More
Adui Mwombee Njaa.

Adui Mwombee Njaa.

Adui ni mwanadamu ambaye hayupo katika upande wa mwanadamu mwenzake yaani asiyekuwa na upendo kwa mwenzie. Njaa ni hali ya kukosa chakula. Sote tunajua kuwa mahitaji muhimu kwa mwanadamu ni chakula, mavazi na mahali pa kuishi. Mavazi na mahali pa kuishi sio muhimu sana ukilinganisha na mahitaji ya chakula kwa sababu bila chakula mtu hawezi kuishi.

Read More
Samaki Mkunje Angali Mbichi!

Samaki Mkunje Angali Mbichi!

Samaki ni kiumbe kinachoishi majini. Mara baada ya kuvuliwa, baadhi ya samaki hutakiwa kukunjwa kwa ajili ya kuhifadhiwa au kwa matumizi ya baadaye. Ili huo mchakato uende vizuri ni lazima samaki hao wakunjwe kulingana na mahitaji ya mlaji. Endapo samaki atakawizwa kukunjwa mara baada ya kuvuliwa, huharibika kiasi kwamba hataweza kukunijka tena.

Read More
Asiyekubali Kushindwa, Si Mshindani!

Asiyekubali Kushindwa, Si Mshindani!

Kwa kawaida kuna mashindano ya aina mbali mbali katika nyanja tofauti tofauti kulingana na mazingira ya sehemu husika.Mtu yeyote anapoingia kwenye mashindano yoyote yale hutegemea kushinda. Lakini inapotokea ameshindwa, hulalamika au kuona kuwa kaonewa. Anasahau kuwa katika mashindano kuna mshindi na mshindwa. Mara zote mshindi huwa ni mmoja tu.

Read More
Muosha Huoshwa!
Swahili Wisdom Swahili Wisdom

Muosha Huoshwa!

Mwosha kwa uelewa wangu ni mtu anayetumika kumwosha maiti na kumuandaa kwa mazishi. Zoezi hili la uoshaji hufanywa zaidi na watu wenye imani ya Dini ya Kiislamu. Kazi ya kuosha maiti huwa ni ngumu kidogo ndio maana inafanywa na watu maalumu. Na mwosha huyo naye akifa huoshwa vile vile na mwosha mwingine. Hayo ndiyo maisha yetu sisi wanadamu.

Read More
Hewala Si Utumwa!

Hewala Si Utumwa!

Hewala ni neno linalomaanisha "ndiyo" au "ni sawa". Hii ina maana ya kukubali na siyo kulazimishwa kama vile ifanyikavyo kwa watumwa. Mtu anaweza kukubali tu ili wafikie suluhu katika kutokukubaliana kwao au kufikia muafaka kuwa basi na yaishe ili amani tipatikane.

Read More
Unaweza Kusahau Maumivu Lakini Sio Tukio!

Unaweza Kusahau Maumivu Lakini Sio Tukio!

Unaweza ukawa na maumivu fulani kama ni ya ugonjwa au maumivu mengine ya maisha. Maumivu hayo yanaweza kuwa ni ya muda fulani au kipindi fulani tu lakini mwisho yakapata jawabu. Katika hali hiyo unaweza ukasahau tu pindi pale linapokuja kupata majibu. Hapo itakuwa sio rahisi tena kukumbuka kama kuna jambo lilikuwa limekutesa. Mfano mzuri ni pale unapokuwa unaumwa lakini ukipona inakuwa sio rahisi tena kukumbuka maumivu uliyokuwa ukipata.

Read More