Muosha Huoshwa!
Swahili Wisdom Swahili Wisdom

Muosha Huoshwa!

Mwosha kwa uelewa wangu ni mtu anayetumika kumwosha maiti na kumuandaa kwa mazishi. Zoezi hili la uoshaji hufanywa zaidi na watu wenye imani ya Dini ya Kiislamu. Kazi ya kuosha maiti huwa ni ngumu kidogo ndio maana inafanywa na watu maalumu. Na mwosha huyo naye akifa huoshwa vile vile na mwosha mwingine. Hayo ndiyo maisha yetu sisi wanadamu.

Read More
Pakacha Kulivunja Nafuu Ya Mchukuzi!
Swahili Wisdom Swahili Wisdom

Pakacha Kulivunja Nafuu Ya Mchukuzi!

Pakacha ni aina ya kapu litumikalo kubebea vitu. Mchukuzi wa kapu hili ni mtu anayebeba mizigo, aidha ikiwa ndani ya pakacha au chombo kingine. Pakacha likijaa vitu linaweza likawa zito lakini jinsi lilivyosukwa linaweza kuruhusu vitu vilivyowekwa humo ndani kuvuja au kumwagika kidogo kidogo wakati vimebebwa na hivyo kupungua kwa uzito ambao humpa ahueni mbebaji /mchukuzi.

Read More