
Mwiba Wa Leo Ndiyo Ua La Kesho!
Mwiba ni sehemu ya mti kwenye tawi ambayo lina ncha kali. Usipokuwa makini inaweza ikakuchoma.
Omba Ufahamu Katika Maisha Yako!
OMBA UFAHAMU KATIKA MAISHA YAKOALFREDA GEORGEUfahamu ni kujua kipi ni kizuri kwako na kipi ni kizuri kwa jamii inayokuzunguka.Hali kadhalika, ufahamu ni kujua kipi ni kibaya kwako na kipi ni kibaya kwa binadamu wenzio ili uweze kukiepuka.Mtu yeyote mwenye ufahamu hutembea katika haki. Hata kama kuna jambo baya, atalihukumu katika haki.Katika maisha, inakupasa ujihukumu mwenyewe kwanza pale unapokuwa umekosea. Usisubiri watu wakuhukumu. Watu wengi wana tabia ya kupenda kuhukumu wenzao na sio kujihukumu wenyewe. Hapo ndipo vurugu na kutokuelewana kunapoanzia. Ni kawaida ya wanadamu kupenda kujitetea kwanza. Ukijua kujihukumu katika yale mabaya unayoyatenda, basi utabadilika. Utakuwa mtu wa kuheshimu kila apitae mbele yako.Usipoweza kujihukumu mwenyewe hautakaa ubadilike, zaidi utawachukia wale ambao wanataka ubadilike. Ukweli ni kwamba, ukiwa na tabia hiyo, hautaishia popote zaidi ya kushindwa.Hatua ya kupata ufahamu, huwa ni ngumu sana kuifikia. Hii ni kutokana na ukweli kwamba kuna vikwazo vingi vya kukutoa katika ufahamu. Hapo ndipo panahitaji uvumilivu maana mambo mengine yatakuudhi na kukukatisha tamaa.Ukibahatika kupata ufahamu, utakuwa umepata kila unachohitaji katika maisha yako. Kwa kawaida, Mungu humtumia mtu mwenye ufahamu na huyo ndiye atakaye sababisha upate kile ambacho umekuwa ukikitamani siku zote. Ili uwe na maisha mazuri, yakupasa uombe kutunukiwa ufahamu na hapo ndipo utakapopata amani.

Maarifa Na Hekima Ni Bora Kuliko Vitambulisho.
Maarifa na hekima vina thamani sana kuliko hicho unachokitafuta. Ukiwa na ufahamu na hekima una zaidi ya fedha. Hii ni kwa sababu ukiwa na huo ufahamu na hekima utafanikiwa kuwa tajiri. Hekima itakuongoza kupata kila unachohitaji katika maisha yako.

Maamuzi Yako Leo Ndiyo Mlango Wako Wa Kutokea Kesho!
Kimaisha, binadamu tunapitia pilikapilika mbalimbali. Nyingine ni za furaha na wakati mwingine ni za huzuni zenye kukatisha tamaa.

Ndege Hai Hula Mchwa, Akifa Naye Huliwa Na Mchwa.
Ndege ni mkubwa kwa umbile ukimlinganisha na mchwa na sisimizi ndio maana anaweza kuwala wadudu hao bila shida. Lakini ndege huyo huyo akifa biashara inabadika. Akifa anakuwa hana ubabe tena, hivyo mchwa na sisimizi nao wanapata ubavu wa kumla.

Pakacha Kulivunja Nafuu Ya Mchukuzi!
Pakacha ni aina ya kapu litumikalo kubebea vitu. Mchukuzi wa kapu hili ni mtu anayebeba mizigo, aidha ikiwa ndani ya pakacha au chombo kingine. Pakacha likijaa vitu linaweza likawa zito lakini jinsi lilivyosukwa linaweza kuruhusu vitu vilivyowekwa humo ndani kuvuja au kumwagika kidogo kidogo wakati vimebebwa na hivyo kupungua kwa uzito ambao humpa ahueni mbebaji /mchukuzi.

Unakimblia Wapi Unapopatwa Na Jambo?
Yako mambo yanayotokea katika maisha ya mtu pasipo yeye mwenyewe kujua. Mambo hayo yanaweza yakawa mazuri au mabaya lakini pengine yeye haelewi nini kinaendelea.

Utayari Una Faida.
Utayari maana yake ni kujitoa kufanya jambo lililokusudiwa na ndio ufunguo wa maisha. Ni ile shauku ya kutaka kufanya jambo na kuzingatia sawasawa na vile unavyoagizwa.Unapozingatia na kutii, ni lazima utakutana na usitawi wako katika kila jambo unalokusudia.

Wembe Ni Mkali Lakini Haukati Mti, Shoka Ni Kali Lakini Haikati Nywele.
Wembe na shoka ni nyenzo zinazotumika kukatia vitu kwa mazingira tofauti. Kwa mfano, wembe unatumika kunyolea.nywele, kukatia kucha na vitu laini. Kwa vyovyote vile, wembe hauwezi kukata mti. Kwa upande mwingine, shoka ni kali na ni nzito lakini haliwezi kunyoa nywele.

Bora Lawama Kuliko Fedheha!
Lawama ni ile hali ya mtu kulalamikiwa ama kushutumiwa kwa kukosa ushirikiano au kupuuza mambo angamizi kwenye jamii. Na fedheha ni ile hali ya kudhalilika au kuaibika kutokana na kutenda jambo lisilokubalika kwenye jamii.

Njia Ya Muongo Ni Fupi!
Mlimbua nchi ni mtu ambaye anaifahamu sana nchi yake. Kwamaneno ya sasa huyu mlimbua nchi tunasema mhujumu wa nchi yaani anaisema vibaya nchi yake; anatoa siri za nchi yake, anaiweka nchi yake katika hali ya hatari kwa namna yeyote anayotaka yeye.

Tunda Jema Halikai Mtini.
Matunda ni aina ya chakula ambayo hulinda miili yetu na magonjwa mbalimbali. Katika mada hii, tunaongelea juu ya tunda ambalo ni moja kati ya matunda mengi yanayosifiwa kuwa ni mema na mazuri. Hii ni wazi tunda lolote lililo zuri haliwezi kukaa sana mtini maana lazima lichumwe mapema na kuliwa.

Jembe Halimtupi Mkulima!
Jembe ni nyenzo inayotumika na mkulima wakati wa kilimo. Kuna majembe ya aina mbalimbali, mfano, jembe la mkono, jembe la kukokotwa na ng'ombe. Hali kadhalika, kuna majembe ya kufungwa na kukokotwa na trekta. Hii yote ni kumwezesha mkulima alime na kupata mazao ya kuridhisha ili aweze kujikimu.

Mkia Ukatikapo Ng'ombe Huona Umuhimu Wake!
Mlimbua nchi ni mtu ambaye anaifahamu sana nchi yake. Kwamaneno ya sasa huyu mlimbua nchi tunasema mhujumu wa nchi yaani anaisema vibaya nchi yake; anatoa siri za nchi yake, anaiweka nchi yake katika hali ya hatari kwa namna yeyote anayotaka yeye.

Mwembe Wa Uwani Nyani Hatambi!
Ni kawaida kwa jamii nyingi kupanda miti ya matunda uwani kwa nyumba zao. Miti ya matunda hii ni kama miparachichi, miembe, mikomamanga na kadhalika. Kwa kufanya hivyo, watu hawa wanakuwa na uhakika wa kupata mavuno na kuyafaidi kwa sababu ndege pamoja na wanyama waharibifu, kama nyani, ngedere nk hawawezi kutamba hapo kutokana na ukweli kwamba wakati wote kunakuwepo na watu. Endapo wanyama hao watakuja, lazima watafukuzwa na wenye matunda.

Mwana Mtukutu Hali Ugali Mkavu!
Wazazi wengi tunabarikiwa na Mungu kupata watoto na ndio furaha kubwa katika ndoa zilizo nyingi. Hata hivyo, wapo wanandoa wengine ambao hawajabarikiwa kupata watoto. Yote ni kazi ya Mungu.

Raha Jipe Mwenyewe!
Furaha ni hali ya kuishi kwa amani na utulivu bila msongo wa mawazo. Msongo wa mawazo ni hali ya kuwa na stress mbalimbali zinazokusumbua katika maisha, kama vile huzuni, kukosa amani na raha, kuwa na mawazo mengi n.k.

Shujaa Haangamizwi Na Mwoga!
Shujaa ni yule mtu ambaye haogopi kuthubutu katika jambo lolote. Hata kama mahali ni pagumu, atajitahidi ili apite au atimize lengo alilokusudia. Mara nyingi mbele yake woga unakuwa haupo. Shujaa huwa anaangalia malengo yake kwa makini.

Angalia Namna Ya Kuongea Kwako.
Lugha inaweza kubadilisha hali ya hewa katika mambo mengi ufanyayo. Matumizi ya lugha yanaweza kubadilisha maisha yako na jamii inayokuzunguka. Maisha ya ndoa yako, kama wewe ni mwanandoa, yanaweza kubadilika pia. Malezi ya watoto yanaweza yakabadilika katika familia zetu kutokana na luga tunazotumia. Lugha kali kwa watoto huwaogopesha kiasi hata kukosa amani na wazazi. Watoto wakiishi kwa woga, wanaweza hata kuingia kwenye makundi mabaya ili kupata faraja. Nyumbani watapaogopa, hawatapenda kukaa na hasa pale mzazi mwenye lugha ya kukera akiwepo. Watoto wakiishi katika mazingira hayo, wanaweza kujifunza mambo yasiyofaa. Wahenga walisema, samaki mkunje angali mbichi, akikauka hakunjiki.

Heshimu Muda Nao Utakuheshimu.
Muda ni kitu cha thamani sana ambacho tumepewa bure na Mwenyenzi Mungu. Kila mtu amepewa bila upendeleo. Kwa kawaida, ukiuheshimu na kuujali muda, nao utakulipa kwani utaona matokeo tatakayokuja kuwa ni mazuri.