Wema Sio Deni, Usisubiri Kulipwa.

Wema Sio Deni, Usisubiri Kulipwa.

Kuna tabia iliyojengeka katika jamii ya kufikiria kuwa unayemfanyia wema ni lazima akulipe. Kuna wale ambao wamesomesha watoto, ndugu na jamaa wengi tu kwa kutegemea kuwa watarudishiwa fadhila kwa wema walioufanya. Kwa bahati mbaya, watu hawa hungojea weee na kukuta hakuna majibu wala fadhila yoyote inayokuja. Hizo huwa ni hisia au mategemeo ya walio wengi.

Read More
Ujuzi Hauzeeki!

Ujuzi Hauzeeki!

Ujuzi ni ufundi au kipaji cha kufanya vitu ili kukuletea faida au kukuingizia kipato. Ujuzi unaweza kupatikana kupitia mafunzo. Hali kadhalika, ujuzi unaweza kutokana na kipaji cha kuzaliwa nacho mtu ambacho kinamuwezesha kufanya vitu vya pekee na vizuri vinavyoweza kununuliwa na watu na hivyo kukupatia kipato.

Read More
Haki Ya Mtu Hailiki!

Haki Ya Mtu Hailiki!

Haki ni kitu halali kinyume cha batili. Mwenye kutoa haki ni Mwenyezi Mungu peke yake, Yeye akisema amesema huwa hakuna wa kumpinga. Mwenyezi Mungu anaweza kuwatumia watu wakupatie haki yako. Mara nyingi tunaona na kuthibitisha ukweli wa usemi huu wa haki ya mtu hailiki bali hucheleweshwa tu.

Read More
Mafanikio Ni Mchakato!

Mafanikio Ni Mchakato!

Kwa kawaida binadamu huwezi kuhesabu mafanikio yako ukiwa umekaa au umebweteka tu. Kama ilivyo kawaida, siku huwa zinabadilika na kila siku ina mambo yake, na mafanikio vivyo hivyo. Lazima upitie mchakato ili uweze kufanikiwa. Endapo mchakato utaonyesha kukukwamishia mafanikio yako, basi elewa huo sio mchakato sahihi. Cha msingi, usikate tamaa endelea kuangalia mchakato mwingine. Unaweza hata kumshirikisha mtu ambaye unamuamini ambaye anaweza akakusaidia kwa mawazo au hata kwa mtaji.

Read More
Maji Hayasahau Ubaridi.

Maji Hayasahau Ubaridi.

Kwa kawaida maji huchemshwa ili yawe ya moto. Lakini taratibu maji hayo hupoa na kurudi kwenye uhalisia wake. Vivyo hivyo, tabia ya mwanadamu huwa haiwezi kujificha kwa muda mrefu bila kurudi kwenye uhalisia wake.

Read More