Mkataa Kwao Mtumwa
Msemo huu unaweza ukamaamisha mtu anayekataa kabila lake, anayekataa utaifa wake na akaweza kuwakataa hata wazazi na ndugu zake pia.
Mpanda Hovyo Hula Hovyo.
Neno mpanda linatokana na neno kupanda. Mpanda ovyo ni yule mtu anayepanda vibaya bila mpangilio. Mtu huyu hupanda bila kufuata hatua zitakiwazo. Mathalani, wakati wa kupanda inatakiwa kuzingatia nafasi kati ya mbegu na mbegu, hali kadhalika, kati ya mstari hadi mstari. Pia inabidi kuzingatia ubora wa mbegu zenyewe ili kupata mavuno yaliyo mengi na bora. La sivyo, kinyume na hapo, mavuno yatakuwa kidogo na yenye ubora duni. Pale mavuno yanapokuwa duni hayatakidhi kuliwa kwa mwaka mzima uliotegewa. Ndio maana ya usemi huu kuwa aliyepanda ovyo, atakula kwa miezi michache tu, kinyume na mategemeo yake.
Nazi Haishindani Na Jiwe!
Nazi ni tunda linalotokana na mti wa mnazi. Kwa kawaida, nazi ni ngumu na jiwe ni kipande kinachotokana na mwamba. Ndio maana tunasema, nazi haiwezi kushindana na jiwe kamwe, kutokana na uimara wa jiwe.
Avuae Nguo Huchutama.
Neno avuae ni kisifa kinachotokana na tendo la kuvua nguo. Msemo huu unamaanisha avuae ni tendo la kuvua nguo na kubaki utupu. Kuchutama ni kuinama kwa ajili ya kuficha utupu.
Akiba Haiozi
Ndege ni viumbe hai na wana mabawa na wana miguu miwili. Wana uwezo wa kuruka. Chakula chao ni wadudu na nafaka.
Tone La Maarifa.
Ukitaka kufanya vizuri maishani wafanyie watu yaliyo mazuri, kwa sababu hakuna namna yoyote ambayo unaweza ukafanikiwa pasipo watu.
Fanya Maamuzi Ukiwa Na Utulivu.
Usifanye maamuzi ukiwa na njaa kali au pochi yako iko tupu. Pale utakaposhiba, utajuta.
Anachoweza Kukufanyia Jogoo Ni Kukupigia Kelele Na Sio Kukutoa Kitandani.
Maisha yetu yanatawaliwa na mambo mengi sana. Mengi tuyafanyayo yanatokana na kufundishwa au kuelekezwa. Katika mambo mengi tunayofundishwa kama tungekuwa tunayatendea kazi tungekuwa mbali sana. Kumbuka kuna mangapi tumesoma ambayo ni ya msingi lakini hatuyafanyii kazi. Huu ndio ukweli wenyewe.
Ukiambiwa Ubaya Wa Mtu, Tafuta Uzuri Wake.
Binadamu tuna tabia moja ya ajabu sana. Mara nyingi tukiambiwa kuwa fulani ni mbaya tunaamini mia kwa mia na kuufanya ubaya wake kuwa ni fimbo ya kumchapia kila uchao. Kila jambo atakalotenda linakuwa ni baya tu kwa jamii inayomzunguka. Ubaya wake unakuwa umekwisha tia mhuri kwenye mioyo ya watu kiasi kwamba hata akipita mahali popote pale atakuwa ni wa kunyooshea vidole tu.
Mafanikio Yanahitaji Kufahamu Na Kukipenda Kile Unachokifanya.
Hapa duniani yako mambo mengi sana tusiyoyajua. Lakini ili tufanikiwe katika jambo fulani lazima tuwe na ufahamu na hilo jambo.
Hujafa Hujaumbika.
Katika maisha tunatambua wazi kuwa Mungu ametuumba na tumekamilika, hata kama hujakamililika katika viungo vingine lakini upo vizuri.
Usiige Wala Kukata Tamaa Ungali Hai.
Mara nyingi sisi,binadamu tunakuwa na tabia ya kukata tamaa ya kuendelea na maisha mara tunapokwama kidogo. Huwa tunasahau kuwa mafanikio hayaji ghafla na kwamba nyuma ya kila fanikio, lazima kuna maumivu makali.
Endelea Kujaribu.
Ni kawaida kabisa kwa mtoto anapotaka kuanza kusimama kushika na kuegemea kila kitu ili kimsaidie asimame. Wakati mwingine anaweza hata kuegemea vitu vya hatari, kama vile chupa ya chai, jiko la moto na vingine vingi tu vinavyokuwa karibu yake. Kwa ujumla, anaweza kushika kitu chochote ambacho kinaweza kuwa ni cha hatari ili mradi tu asimame.
Donda La Kichwa Mkaguzi Mkono!
Ni ukweli usiopingika kuwa kila binadamu lazima atakuwa na mtu au watu wa karibu ambao huwa ni tegemeo lake katika mambo mengi ayatendayo, hususani wakati wa shida ama wakati wa raha. Wako watu ambao wanaweza kuwa karibu zaidi kiasi kwamba kunakuwa hakuna jambo unalowezakulifanya bila wao kujua au kuchangia mawazo.
Wajibika Na Maisha Yako
Hapa duniani, kila mtu anatakiwa kupambania maisha yake. Unaposimamia na kudhibiti shughuli zako mwenyewe utaridhika, utapata amani, furaha na faida.
Usilaumu Kimbunga, Tunza Mkeo.
Siyo jambo geni kwenye jamii zetu kusikia kuwa jukumu na wajibu wa msingi wa kila mwanaume ni kumtunza mke wake kwa kumpatia mahitaji yake ya msingi. Lakini maisha yamebadilika na hivyo kufanya majukumu yabadilike pia. Hii ni kutokana na hali ngumu ya maisha. Kwa kiasi kikubwa, wanawake wengi wamekuwa wakilalamikia wanaume kusahau majukumu yao. Hii imesababisha ndoa nyingi kuvunjika.
Usipime Mafanikio Yako Na wale Walio Kuzidi.
Mipango ya watu wengi huwa ni ya kuleta mafanikio na sio vinginevyo. Unapoweka mipango yako unaweka na mikakati ya jinsi ya kutekeleza hiyo mipango. Mikakati hiyo itatakiwa iwe na uwezeshaji, inawezekana kifedha au kimawazo. Kama ni kifedha, unaweza kutumia njia ya kukopa au vinginevyo. Kama ni kimawazo, utahitaji kupata mawazo kutoka kwa watu mbalimbali, watu wenye busara na uungwana.
Ujinga Mzigo!
Tujikumbushe kwanza hilo neno ujinga ni nini. Ujinga ni ile hali ya mtu asiyejitambua au kukosa ufahamu wa kufanya jambo lolote lenye manufaa au faida kwa kutumia akili zake mwrnyewe. Bila shaka tunajionea wenyewe jinsi Serikali yetu inavyojitahidi kutoa elimu bure kwa watoto wetu na hata kutoa mikopo kwa vijana wetu wanaoingia Chuo Kikuu. Lengo kuu la kufanya hivyo kuwapa elimu ili kufuta ujinga. Taifa linatakiwa liwe na watu wenye maarifa, uelewa na uwezo wa kujitambua wa kufanya shughuli za maendeleo ya taifa lao wakiwa na uelewa zaidi.
Jaribu Kutengeneza Utajiri Na Siyo Pesa!
Kuna msemo mwingine ambao unasema “Mwenye Pesa Siyo Mwenzio .”Ukiangalia kwa undani kabisa utashuhudia huo msemo kuwa ni kweli lakini swali la kujiuliza ni muda ambao pesa hizo hudumu. Tumeona kwa macho yetu watu wakifilisika na kubaki kama vile walivyokuwa mwanzo. Haya yote hutokea kwa ile dhana ya kufikiria kuwa pesa ndio kila kitu.
Haijawahi Kutokea Mbwa Akaitwa Mbwa Akawa Kichaa.
Katika maisha unaweza ukaitwa majina mengi tu, mengine ya maudhi, mengine ya kufurahisha, ili mradi tu, utabandikwa majina ya kila aina.!Katika majina hayo, yawezekana mengine yakakuharibia au kukubadilishia tabia yako ambayo tokea mwanzo ilikuwa nzuri.