Sikio la Kufa Halisikii Dawa

Caroline Swai - Wisdom&Wellness Counselor (TEWWY)

Masimulizi ...

by Caroline Swai (Wisdom&Wellness Counselor - TEWWY).

Siku zote yeyote asiyesikia analoambiwa na wakubwa zake huishia pabaya. Mtoto mmoja tangu akiwa mdogo alianza tabia ya udokozi akiwa nyumbani kwao. Wazazi walimkanya lakini hakusikia. Aliendelea na tabia hiyo ya wizi kwa majirani na shuleni, alikanywa na waalimu wake, napo pia hakusikia. Alipomaliza darasa la saba alifaulu lakini akachagua kuendelea na tabia yake ya wizi. Aliamua kujiunga na makundi mabaya, makundi ya majambazi wenye uzoefu. Siku moja walienda kuiba benki, kwa bahati mbaya yule kijana alipigwa risasi na kufariki pale pale, wenzake wazoefu walitoroka. Wazazi wake walisikitika sana kumkosa mtoto wao. Lakini wana jamii walisikika wakisema ama kweli sikio la kufa halisikii. Endapo angewasikiliza wazazi na wote waliomkanya tangu utoto wake, haya yote yasingemkuta. Kwa upande wa jamii na taifa, nguvu kazi ilipotea kwenye nyanja za kielimu, kiuchumi na kisiasa. Kisa hiki kina funzo kubwa kwa vijana wetu. Yawapasa wawe wasikivu, wazingatie yale wanayoaswa na wakubwa zao kwani "asiyesikia la mkuu huvunjika guu".



The Healing Hands Project

We are excited to launch the #HealingHands project. The project supports interpersonal counseling, group talk therapy and psychoeducation resources to be delivered through arts, where clients learn to handcraft traditional beaded jewelry as a marketable skill. It also promotes the economic growth of grandmothers who are trained in and are implementing WHO's mental health Gap Action Program #mhGAP. Income generated from sales of the jewelry will also support the sustainable implementation of accessible psychosocial interventions among underserved communities. Follow us @TEWWYWisdom @WisdomWellnessCollection to stay posted.

#MentalHealth #Grandmother #Wisdom #Wellness #ArtTherapy

Previous
Previous

Mtaka Yote Kwa Pupa Hukosa Yote

Next
Next

Kushinda na Kushindwa ni Sehemu ya Maisha ya Binadamu