Asiyefunzwa na Mamaye, Hufunzwa na Ulimwengu

Masimulizi ...
by Tap Elderly Women's Wisdom for Youth (TEWWY).
Ni jukumu la wazazi kuwapa malezi mazuri na mema watoto wao. Mwalimu wa kwanza wa mtoto ni wazazi. Malezi haya yanatakiwa yaanze tokea siku ya kwanza mtoto anazaliwa. Ikumbukwe kuwa mtoto anapozaliwa anakuwa kama karatasi nyeupe kabisa isiyo na doa ama alama yoyote. Mzazi/mwezi anakuwa wa kwanza kabisa kuandika katka karatasi ile nyeupe. Akianza kwa kuandika mambo yasiyofaa yatabaki kwenye karatasi ile. Hali kadhalika akiandika mambo mazuri pia yatabakia kwenye hiyo karatasi. Huo ndio mwanzo wa kumjenga mtoto, vizuri ama vibaya. Kwa maana nyingine, utakavyomlea mtoto wako ndivyo atakavyokuwa, mathalan kuwa na adabu njema kwa watu ama kutokuwa na adabu, kuwa jeuri kwa watu ama kuwa mtii, kuwa na nidhamu ama kuwa mtovu wa nidhamu
Ni rahisi sana kwa watu wamuonapo mtoto kwa mara ya kwanza kujua malezi aliyopata. Matendo na maneno ya mtoto aliyelelewa vizuri ni tofauti sana na ya yule aliyelelewa vibaya. Mathalani, kama mtoto ameanza kuonyesha tabia mbaya kama ya utovu wa nidhamu na wazazi wakamwacha tu aendelee kukosa adabu, huko hakutakuwa ni kumpenda; ni kumdhuru. Kwani mtoto huyo akija kuwakosea watu wengine, hawatamuachia. Watampiga, na pengine vibaya zaidi kuliko ambavyo wangalimpiga wao wenyewe pale alipokuwa mdogo. Mara nyingi mafunzo ya ulimwengu ni ya kikatili, hayana huruma hata kidogo.
Kuna mipaka katika kuwapenda watoto wetu. Tusiwaharibu kwa kisingizio cha kuwapenda kwani tukifanya hivyo tutakuja kujuta pale ulimwengu unapochukua nafasi yetu ya kuwafunza kama wazazi. Na ikifikia hatua mtoto akaambiwa maneno haya ya asiyefunzwa na mama hufunzwa na ulimwengu, na bahati mbaya endapo wazazi
wakayasikia, wanaweza kuumia sana kwani pamoja na kwamba yanaelekezwa kwa mtoto, mzazi pia analaumiwa. Haiwi lawama kwa mtoto tu bali na kwa wazazi pia ambao mnaonekana dhahiri mlishindwa kutimiza wajibu wenu kama wazazi.
Somo hili ni zuri kwa watoto na kwa wazazi pia, hali kadhalika, na kwa wale ambao hukataa kusikiliza maoni au ushauri wa wengine kwani mwisho wa siku huangukia kwenye mikono ya walimwengu.
Hima wazazi tutimize wajibu wetu kama wazazi; hali kadhalika watoto mzingatie malezi ya wazazi ili msije mkaingia kwenye darasa la walimwengu.
The Healing Hands Project
The Healing Hands project will economically empower people to achieve financial autonomy by building entrepreneurial skills and embedding skills transfer within the community - eliminating poverty as a driver of ill mental health. Funds raised from the jewelry will help sustain the implementation of accessible psychosocial interventions in underserved communities and promote the economic empowerment of the grandmothers who have been trained in and are implementing WHO's mental health Gap Action Program. Healing Hands provides interpersonal counseling, group talk therapy, and psychoeducation resources delivered through arts, where clients learn to handcraft traditional beaded jewelry as a marketable skill. Follow us @TEWWYWisdom @WisdomWellnessCollection to stay up-to-date.
#MentalHealth #Grandmother #Wisdom #Wellness #mhGAP #HealingHands #Art #Culture #Tanzania