Ulegevu Umebeba Umaskini

Simulizi
by Alfreda George (Wisdom&Wellness Counselor - TEWWY).
Watu wengi tuna tabia ya kulalamika sana kuhusu maisha kuwa magumu. Ukifuatilia sana utakuta wale wenye malalamiko ya aina hii ni wale ambao hawataki kutoka kwenye visanduku vyao vya uvivu.
Kusema kweli, ziko fursa nyingi tu ambazo zinaweza kutupatia kipato. Tatizo letu kubwa ni kuchagua kazi za kufanya. Kuna kazi nyingine watu huzionea aibu kuzifanya. Pengine ni kwa kwa sababu wanajiona kwamba wamesoma sana na hivyo hawawezi kufanya kazi ndogo ndogo na za hali ya chini. Wao wanajiona ni matawi ya juu lakini ukweli ni kwamba wako sawa na watu wengine.
Vijana wengi wanasumbuliwa sana na mawazo haya. Zipo shuhuda nyingi zinazoweza kuthibitisha ukweli huu. Kwa sababu ya uvivu walionao hushindwa kujiongeza au kuangalia njia mbadala za kuweza kujikimu kwa mahitaji yao ya msingi. Haina maana hawana uwezo wa kufikiri na kutenda, bali uvivu wa kuchukua hatua ndio umekuwa ugonjwa wao mkuu. Vijana wengi ni walegevu sana wanataka kazi nyepesi nyepesi lakini zenye malipo makubwa. Hata katika vitabu vitakatifu vimeandika tusifanye kazi kwa ulegevu. Kazi yeyote tuifanyayo yatupasa tuitendee haki, tuifanye kwa bidii zote na kwa ufanisi.
Hali kadhalika, vitabu vitakatifu vinanena, “amelaaniwa yule afanyaye kazi kwa ulegevu kwani kwa kufanya hivyo anakaribisha umaskini”. Umaskini sio ugonjwa, na wala hakuna aliyeandikiwa umaskini. Umaskini huletwa na ulegevu pamoja na uvivu ambao binadamu tulio wengi tunao. Mazingira tunayoishi yanaweza kuwa magumu. Yatulazimu tuendane na mazingira yanayotuzunguka ili tuweze kumudu maisha yetu. Inatupasa kuwaelekeza
vijana hali halisi ya maisha kuliko kuwaacha waendelee kujishughulisha na utandawazi ambao kwa kadri siku zinavyozidi kwenda, ndivyo tunavyowaona wakichanganyikiwa na hatimaye kushindwa kujua lipi jema na lipi baya. Dunia imekuwa kijiji sasa hivyo kuiga yanayoendelea huko majuu kwa walioendelea, imekuwa ni mtindo wa maisha ya vijana wengi. Kwa hakika, vijana wengi wanaishia pabaya. Ni lazima tuwasaidie ili waweze kuwa na uwezo wa kuchagua na kutenganisha kati ya mema na mabaya. Wanajitaji msaada wetu.
The Healing Hands Project
The Healing Hands project will economically empower people to achieve financial autonomy by building entrepreneurial skills and embedding skills transfer within the community - eliminating poverty as a driver of ill mental health. Funds raised from the jewelry will help sustain the implementation of accessible psychosocial interventions in underserved communities and promote the economic empowerment of the grandmothers who have been trained in and are implementing WHO's mental health Gap Action Program. Healing Hands provides interpersonal counseling, group talk therapy, and psychoeducation resources delivered through arts, where clients learn to handcraft traditional beaded jewelry as a marketable skill. Follow us @TEWWYWisdom @WisdomWellnessCollection to stay up-to-date.
#MentalHealth #Grandmother #Wisdom #Wellness #mhGAP #HealingHands #Art #Culture #Tanzania