Mcheza Kwao Hutunzwa.

Mcheza Kwao Hutunzwa.

Mcheza kwao ni mtu ambaye anajishughulisha sana na mambo yanayofanyika kwenye jumuiya yake. Kutunzwa ni kupewa tuzo/zawadi pale atakapofanikisha jambo. Kiubinadamu huwa ni jambo zuri kutambuliwa mchango wao pale mtu afanyapo vizuri, iwe ni kwenye jumuia, masomo, kilimo ama eneo la kazi. Hata katika familia, inatakiwa zawadi zitolewe kwa wana familia.

Read More
Adui Mwombee Njaa.

Adui Mwombee Njaa.

Adui ni mwanadamu ambaye hayupo katika upande wa mwanadamu mwenzake yaani asiyekuwa na upendo kwa mwenzie. Njaa ni hali ya kukosa chakula. Sote tunajua kuwa mahitaji muhimu kwa mwanadamu ni chakula, mavazi na mahali pa kuishi. Mavazi na mahali pa kuishi sio muhimu sana ukilinganisha na mahitaji ya chakula kwa sababu bila chakula mtu hawezi kuishi.

Read More
Hewala Si Utumwa!

Hewala Si Utumwa!

Hewala ni neno linalomaanisha "ndiyo" au "ni sawa". Hii ina maana ya kukubali na siyo kulazimishwa kama vile ifanyikavyo kwa watumwa. Mtu anaweza kukubali tu ili wafikie suluhu katika kutokukubaliana kwao au kufikia muafaka kuwa basi na yaishe ili amani tipatikane.

Read More
Unaweza Kusahau Maumivu Lakini Sio Tukio!

Unaweza Kusahau Maumivu Lakini Sio Tukio!

Unaweza ukawa na maumivu fulani kama ni ya ugonjwa au maumivu mengine ya maisha. Maumivu hayo yanaweza kuwa ni ya muda fulani au kipindi fulani tu lakini mwisho yakapata jawabu. Katika hali hiyo unaweza ukasahau tu pindi pale linapokuja kupata majibu. Hapo itakuwa sio rahisi tena kukumbuka kama kuna jambo lilikuwa limekutesa. Mfano mzuri ni pale unapokuwa unaumwa lakini ukipona inakuwa sio rahisi tena kukumbuka maumivu uliyokuwa ukipata.

Read More

Omba Ufahamu Katika Maisha Yako!

OMBA UFAHAMU KATIKA MAISHA YAKOALFREDA GEORGEUfahamu ni kujua kipi ni kizuri kwako na kipi ni kizuri kwa jamii inayokuzunguka.Hali kadhalika, ufahamu ni kujua kipi ni kibaya kwako na kipi ni kibaya kwa binadamu wenzio ili uweze kukiepuka.Mtu yeyote mwenye ufahamu hutembea katika haki. Hata kama kuna jambo baya, atalihukumu katika haki.Katika maisha, inakupasa ujihukumu mwenyewe kwanza pale unapokuwa umekosea. Usisubiri watu wakuhukumu. Watu wengi wana tabia ya kupenda kuhukumu wenzao na sio kujihukumu wenyewe. Hapo ndipo vurugu na kutokuelewana kunapoanzia. Ni kawaida ya wanadamu kupenda kujitetea kwanza. Ukijua kujihukumu katika yale mabaya unayoyatenda, basi utabadilika. Utakuwa mtu wa kuheshimu kila apitae mbele yako.Usipoweza kujihukumu mwenyewe hautakaa ubadilike, zaidi utawachukia wale ambao wanataka ubadilike. Ukweli ni kwamba, ukiwa na tabia hiyo, hautaishia popote zaidi ya kushindwa.Hatua ya kupata ufahamu, huwa ni ngumu sana kuifikia. Hii ni kutokana na ukweli kwamba kuna vikwazo vingi vya kukutoa katika ufahamu. Hapo ndipo panahitaji uvumilivu maana mambo mengine yatakuudhi na kukukatisha tamaa.Ukibahatika kupata ufahamu, utakuwa umepata kila unachohitaji katika maisha yako. Kwa kawaida, Mungu humtumia mtu mwenye ufahamu na huyo ndiye atakaye sababisha upate kile ambacho umekuwa ukikitamani siku zote. Ili uwe na maisha mazuri, yakupasa uombe kutunukiwa ufahamu na hapo ndipo utakapopata amani.

Read More