Mtizamo Chanya Ni Muhimu Katika Maisha

Simulizi
by Victoria Nakajumo (Wisdom&Wellness Counselor - TEWWY).
Kati ya vitu vinavyotupotezea muda watu wengi, ni ile hali ya kutaka kujua watu gani wanatusema vibaya. Yaani unatumia muda wako mwingi kutafuta habari mbaya zinazosemwa kuhusu wewe kuliko muda unaoutumia kufanya mambo yako ili kutimiza malengo yako.
Unakuta muda wako wote unajihisi kuwa unasemwa vibaya, ukiona watu wawili wamekaa wanaongea unahisi wanakujadili wewe na kukusema vibaya, ukiona mtu wako wa karibu anaongea na simu unajificha kusikiliza ukihisi unaongelewa wewe.
Ndugu au mwenzi wako akiweka simu unaichukua na kuanza kuikagua kama kuna namna unasemwa kwa watu vibaya. Maisha ya namna hiyo siyo mazuri, ni mabaya, na si hivyo tu, yatakukosesha furaha na amani na hatimaye utashindwa kujiamini. Amua kuishi maisha ya furaha, maisha ya kujiamini, kwa sababu haijalishi wewe unaona umekamilika kiasi gani ama ni bora kuliko watu wengine kwa kiasi gani. Binadamu ameumbwa kusemwa na watu, anaweza kusemwa kwa mazuri ama kwa mabaya, yote yanawezekana. Siyo rahisi hata kidogo kuwazuia watu kukusema. Ni kawaida kusemwa na wala usitishike. Hatuna mamlaka ya kupanga nini kisemwe dhidi yetu. Chochote kinaweza kusemwa juu yako. Cha msingi, kama wewe ni mtu mzuri/mwema maneno ya watu, yawe mabaya ama mazuri hayatakufanya wewe kuwa mbaya. Hali kadhalika, maneno yoyote mazuri, yatakayosemwa juu yako hayatakufanya wewe kuwa mzuri. Kama wewe ni mbaya, utabaki kuwa mbaya tu. Cha msingi, yatupasa tujitahidi kuishi maisha yanayokubalika mbele za watu na mbele za Mungu. Mengine yawayo yote, huwezi kuyazuia.
Watu watabaki kuwa watu, na si vinginevyo. Wekeza muda wako kuyatenda yaliyo mema, timiza kusudi lako la hapa duniani. Tukumbuke kuwa muda tuliopewa kuishi hapa duniani ni mfupi sana, una kikomo. Hatukuja kuishi milele hapa duniani. Ukianza kuhangaika kila siku kutafuta mbaya wako ni nani, na nani wanakusema vibaya, hutafika kule unakotaka kufika. Utashindwa kutimiza malengo yako.
Kuanzia leo jitahidi kubadili mtazamo wako juu ya vitu na watu. Jitahidi kuwa na mtazamo chanya. Maisha ndivyo yalivyo.
The Healing Hands Project
The Healing Hands project will economically empower people to achieve financial autonomy by building entrepreneurial skills and embedding skills transfer within the community - eliminating poverty as a driver of ill mental health. Funds raised from the jewelry will help sustain the implementation of accessible psychosocial interventions in underserved communities and promote the economic empowerment of the grandmothers who have been trained in and are implementing WHO's mental health Gap Action Program. Healing Hands provides interpersonal counseling, group talk therapy, and psychoeducation resources delivered through arts, where clients learn to handcraft traditional beaded jewelry as a marketable skill. Follow us @TEWWYWisdom @WisdomWellnessCollection to stay up-to-date.
#MentalHealth #Grandmother #Wisdom #Wellness #mhGAP #HealingHands #Art #Culture #Tanzania