MTAKA NYINGI NASAHA, HUMKUTA MINGI MISIBA

Sakina Bushiri
Wisdom&Wellness Counselor
Mangaya, Dar-es-Salaam
Hii hutumika kuwaasa wale wanaopenda kufanya urafiki na kila mtu au kuwafanya kama ndugu zao hukutwa na misiba mingi kwani kila tatizo la mmoja wao litamhusu yeye pia.
Msemo huu unaweza kutumika kwa watu ambao wanapenda kujionyesha ni maarufu na hivyo kutaka waonekane wanashiriki kila jambo litokealo, ukweli ni kwamba siyo rahisi kuwepo kila mahali.