Mtoto Umleavyo Ndivyo Akuavyo

Margaret Kayombo - Wisdom&Wellness Counselor (TEWWY)

Masimulizi ...

by Margaret Kayombo (Wisdom&Wellness Counselor - TEWWY).

Fundisho kwa watoto na vijana: “Muwe watii na heshima kwa wazazi wenu”

Palikuwa na mtoto mmoja aliyekuwa anaitwa Ipyana ambaye alikuwa mtukutu na mwenye ghadhabu. Siku moja alimwomba baba yake pesa ili aende kutalii nchi mbalimbali ulimwenguni kwa gharama kubwa. Baba yake alimsihi sana mwanawe asiondoke, lakini Ipyana hakusikia na aliamua kuondoka. Alizunguka huku na huko akiangalia maghorofa, pwani na wanyama kama vile Twiga na huku akitumia pesa ovyo. Miaka ilizidi kwenda lakini Ipyana hakukumbuka kurudi nyumbani, alifurahia mambo mengi mapya na ya kustaajabisha.

Wazazi wake waliona bora wamtafute mtoto wao huenda huko alikoenda alipatwa na masaibu mazito. Walikwenda kila kona lakini hawakufanikiwa kumpata. Kazi nzito na ngumu ilikuwa mbele yao. Kila walikofika, waliambiwa alikuwa hapa lakini alikwishaondoka kwenda nchi nyingine. Wazazi wake walikata tamaa na kusononeka sana. Hatimaye waliamua kurudi nyumbani.

Ipyana alikuwa amewatwisha mzigo mzito mioyoni mwao, mzigo wasioweza kujitua. Waliumia na kukerwa sana na suluba inayosabishwa na mtoto wao. Kutokana na matumizi yake mabaya ya pesa, aliishiwa. Maisha yalibadilika, yakaanza kuwa ya shida. Alianza kukonda kwa sababu ya kukosa lishe. Nguo zake zilianza kumpwaya kabisa. Alihangaika huku na huko kutafuta chakula bila mafanikio. Kwa kuwa alikuwa mtoto mtukutu, watu hawakumsaidia kabisa, akabaki mpweke. Hatimaye alifanya maamuzi ya busara ya kurudi nyumbani kwa wazazi wake ili kuomba msamaha.

Kwa mzazi mtoto ni mtoto, msamaha huwepo daima. Ni sawa na usemi tuliozoea kuusikia: “mkono wako ukishika uchafu huwezi kuukata”, ndivyo ilivyokuwa kwa kijana Ipyana, wazazi wake hawakumtupa, walimsamehe.

Tangu siku hiyo Ipyana alibadili mwenendo wake na kuwa mtoto mwema katika kila jambo.

Hadithi hii ina masomo mawili kwa wazazi, moja, tuchunguze tabia za watoto wetu kuanzia mapema kabisa, na tuwakemee watoto wanapoanza kubadilika. Pili, wazazi tusiridhie kila aombacho mtoto, ni lazima kupima kwanza na kuangalia manufaa ya hicho anachoombea fedha mtoto wako. Pengine Ipyana asingepewa fedha na wazazi wake asingeweza kuondoka na kukutwa na masahibu aliyoyapata.

Kazi kwetu wazazi, tusidekeze watoto bila sababu. Tusiwalee watoto wetu kihasara hasara. Tusichangie kuwaharibu watoto wetu kwa kisingizio cha kuwapenda.

The Healing Hands Project

The Healing Hands project will economically empower people to achieve financial autonomy by building entrepreneurial skills and embedding skills transfer within the community - eliminating poverty as a driver of ill mental health. Funds raised from the jewelry will help sustain the implementation of accessible psychosocial interventions in underserved communities and promote the economic empowerment of the grandmothers who have been trained in and are implementing WHO's mental health Gap Action Program. Healing Hands provides interpersonal counseling, group talk therapy, and psychoeducation resources delivered through arts, where clients learn to handcraft traditional beaded jewelry as a marketable skill. Follow us @TEWWYWisdom @WisdomWellnessCollection to stay up-to-date.

#MentalHealth #Grandmother #Wisdom #Wellness #mhGAP #HealingHands #Art #Culture #Tanzania

Previous
Previous

Majivuno na Kiburi ni Adui wa Maendeleo

Next
Next

Aanguaye Huanguliwa