Majivuno na Kiburi ni Adui wa Maendeleo

Masimulizi ...
by Margaret Kayombo (Wisdom&Wellness Counselor - TEWWY).
Katika maisha ya mwanadamu hapa duniani majivuno na kiburi ni kikwazo cha kukurudisha nyuma kimaendeleo.
Katika nchi moja kulikuwa na mfalme mmoja mwenye maringo na dharau sana, aliwaona watu wake kama sio binadamu. Raia wake walikuwa wanamchukia sana, hata wakamwombea afe. Siku moja alipokuwa anahutubia kwenye mkutano wa wazee alithubutu kusema kuwa yeye hajawahi kuiona njaa na angefurahi sana kama angempata mtu ambaye angeweza kumuonyesha njaa ilipo na inafananaje, kwani huwa anasikia tu kuwa duniani kuna njaa.
Wazee walikasirishwa sana na kauli zake hizo za mara kwa mara. Ndipo mzee mmoja mwenye busara akajitolea na kwenda kumweleza mfalme ya kuwa, yeye yupo tayari kumpeleka na kumwonyesha njaa ilipo, Mfalme alikubali kwenda na huyo mzee ili akaione njaa kwa macho yake.
Mzee yule alitengeneza mikate yake saba na akamwambia mfalme kuwa safari imejiri. Pia alimwambia mfalme asichukue kitu chochote, kwani yeye angechukua kila kitu cha lazima pamoja na chakula kwa ajili ya safari yao. Hali kadhalika, alimwambia kuwa hawatatumia chombo chochote cha usafiri, itawabidi waende kwa miguu, maana huko kwenye njaa hakuendeki na gari, njia pekee ni ya miguu tu.
Siku ya kuondoka ilipowadia, walianza safari alfajiri na mapema. Wakaenda mbali sana na kwa vile mfalme hakuzoea kutembea, ilipofika saa sita akawa amechoka ile mbaya. Njaa nayo ikawa inamuuma sana. Yule mzee akafungua mikate yake na kuanza kula peke yake. Kwa vile njaa haina adabu, Mfalme alimuomba kipande cha mkate lakini yule mzee alimnyima. Kwa kebei alimwambia kuwa yule ambaye anasafiri kwenda kuiona njaa huwa hali chochote. Mfalme alivumilia na baada ya kupumzika waliendelea na safari. Ilipofika jioni, maskini mfalme akashindwa kuendelea na safari na kuomba chakula kwa yule mzee.
Baada ya kumuona mfalme yuko hoi bin taaban, yule mzee kwa taratibu alimjibu swali lake mfalme la wapi njaa ilipo. Alimwambia: “hakuna mahali maalumu ambapo ni maskani ya njaa, bali ile anayoihisi ndiyo njaa yenyewe”. Aliendelea kwa kusema: “njaa inamfanya mtu yeyote asiwe na nguvu”. Hivyo yule mzee alimsihi mfalme aweke ahadi kama hatarudia tena vitendo vyake vya majivuno na dharau kwa watu. Asipofanya hivyo kwa kuweka nadhiri yule mzee
atamwacha palepale ili afe kwa njaa. Kutokana na alivyokuwa anajisikia mfalme, wosia wa mzee huyu ulimfanya atii na kuufuata. Mfalme aliapa kwa Mungu kuwa hatarudia tena kuringa, kudharau na kukufuru kama alivyokuwa amezoea.
Hapa tunajifunza mengi nayo ni:
- Kama umejaliwa kuwa na utajiri, yakupasa umshukuru Mungu, usiwadharau wale ambao hawana.
- Usitumie madaraka uliyopewa kwa ajili ya kuwanyanyasa wengine.
- Tuwe na unyenyekevu kwa kila mtu ili siku tutakapopata matatizo wawepo wa kutusaidia..
Hadithi hii inafanana na msemo huu: ‘Adui yako muombee njaa’.
Hapa tumeona pamoja na madaraka aliyokuwa nayo mfalme njaa ilimfundisha kuwa na adabu na utu na hatimaye kuacha majivuno.
The Healing Hands Project
The Healing Hands project will economically empower people to achieve financial autonomy by building entrepreneurial skills and embedding skills transfer within the community - eliminating poverty as a driver of ill mental health. Funds raised from the jewelry will help sustain the implementation of accessible psychosocial interventions in underserved communities and promote the economic empowerment of the grandmothers who have been trained in and are implementing WHO's mental health Gap Action Program. Healing Hands provides interpersonal counseling, group talk therapy, and psychoeducation resources delivered through arts, where clients learn to handcraft traditional beaded jewelry as a marketable skill. Follow us @TEWWYWisdom @WisdomWellnessCollection to stay up-to-date.
#MentalHealth #Grandmother #Wisdom #Wellness #mhGAP #HealingHands #Art #Culture #Tanzania