Hivi Ulivyo Ni Matokeo Ya Uliyojinenea

Simulizi ...
by Alfreda George (Wisdom&Wellness Counselor - TEWWY).
Mara nyingi tunasikia watu wakisema ‘kinywa kinaumba’. Wengi hupenda kuamini kuwa maisha ya mtu yanatengenezwa na vile mtu anavyojipangia na anavyojinenea mwenyewe. Hii ina maana kuwa binadamu ana mamlaka ya kupanga/kuamua maisha yake yaweje. Lakini haina maana kuwa yale mazuri uliyojinenea yatatokea bila kuweka jitihada zozote, la hasha. Mfano ukijinenea kwa kusema kuwa mimi nitakuwa tajiri”, itakupasa utende matendo yatakayokufanya ufikie hayo uliyonena, kama kufanya kazi kwa bidii nk. Hivyo hivyo, ukijinenea kuwa utakuwa daktari, itakupasa ukazane kusoma kwa bidii, hususani masomo yatakayokuwezesha kufikia ndoto hiyo ya kuwa daktari. Hakuna mafanikio yatakayodondoka kutoka juu, hiyo itakuwa ndoto ya mchana
Hata kwenye malezi ya watoto wetu ni muhimu sana kuangalia maneno tunayowanenea watoto wetu kwani mara nyingi watoto huja kuwa hivyo walivyonenewa ama walivyotabiriwa na wazazi wao. Mathalani, unaweza kumwambia mtoto wako maneno kama: “wewe mtoto hutafanikiwa katika maisha yako”. Pengine unaposema haya unakuwa kama unatania. Lakini kumbe maneno haya yanakuja kumfanya mtoto awe vile ulivyomtamkia. Hii ni kutokana na jinsi ulivyokuwa unamtamkia katika malezi yake. Hali kadhalika pale unapomwambia mtoto wewe ni mjinga basi mtoto atakuwa hivyo. Kwa maana kimtokacho mtu ndicho kiumbikacho katika maisha ya mwanadamu ya kila siku.
Kwa ujumla usijinenee mambo hasi wewe mwenyewe, uzao wako na hata watu wengine. Usifikirie au kuzungumzia kushindwa daima bali ongelea masuala ya ushindi. Ni lazima kujiamini.
Mathalani, shirika la TEWWY linaweza likawa linapitia magumu mengi na hivyo kushindwa kutekeleza majukumu yake. Pamoja na magumu yote linayoyapitia, yatupasa tuseme TEWWY itashinda kwa maana tumedhamiria kufanya hivyo. Ruhusu mdomo wako uongelee mambo yaliyo chanya na sio hasi. Mambo huwa vile mlivyojinenea, kama mmeomba na kutamka ushindi, basi mtashinda, na kama mmetamka kushindwa, basi mtashindwa. Hata wewe hivyo ulivyo ni matokeo ya yale uliyojinenea wewe mwenyewe.
Mara nyingi mambo mengi yanayotupata ni matokeo ya yale tuliyojinenea ama kujitamkia. Hata watoto wetu wanakuwa vile walivyo kutokana na jinsi tulivyokuwa tunawatamkia katika malezi yao. Pale unapomwambia mtoto wewe ni mjinga basi atakuwa hivyo. Kwa maana kimtokacho mtu ndicho kiumbikacho katika maisha ya kila siku.
Kwa ujumla usijinenee mambo hasi wewe mwenyewe na hata uzao wako. Usikiri kushindwa, daima ongelea kushinda. Mathalani, TEWWY inasema lazima tutashinda kwa sababu tumedhamiria kushinda. Acha mdomo uongelee mambo chanya na sio mambo hasi asilani.
The Healing Hands Project
The Healing Hands project will economically empower people to achieve financial autonomy by building entrepreneurial skills and embedding skills transfer within the community - eliminating poverty as a driver of ill mental health. Funds raised from the jewelry will help sustain the implementation of accessible psychosocial interventions in underserved communities and promote the economic empowerment of the grandmothers who have been trained in and are implementing WHO's mental health Gap Action Program. Healing Hands provides interpersonal counseling, group talk therapy, and psychoeducation resources delivered through arts, where clients learn to handcraft traditional beaded jewelry as a marketable skill. Follow us @TEWWYWisdom @WisdomWellnessCollection to stay up-to-date.
#MentalHealth #Grandmother #Wisdom #Wellness #mhGAP #HealingHands #Art #Culture #Tanzania