Misukosuko Huleta Mafanikio

Alfreda George - Wisdom&Wellness Counselor (TEWWY)

Simulizi

by Alfreda George (Wisdom&Wellness Counselor - TEWWY).

Maisha ya binadamu hayana formula maalum. Mara nyingi kwenye maisha, kufanikiwa kwa mtu hutegemea sana na uwepo wa jambo ambalo litamsukuma ili aweze kubadili taratibu za maisha yake. Kwa mfano, kuna watu ambao wanaona kuishi na mtu bila kulipa chochote ndio chanzo chao cha kufikia malengo yao. Ukweli ni kwanba watu wenye mawazo ya namna hiyo huishia kushindwa vibaya. Watu wa roho tegemezi hawawezi kuona kuwa wanatakiwa kufanya mambo yao wenyewe ili waweze kujitegemea.

Vijana wengi wa siku hizi ndivyo walivyo. Hupenda sana maisha ya dezo, maisha ya bure bure. Hawataki maisha ya kuanzia chini. Hupenda kuwa na mambo makubwa ambayo yako nje ya uwezo wao, mambo ya mkato. Tatizo kubwa ni kwamba hawajui kuwa hao wanaoonekana sasa hivi kuwa wanajiweza, wametoka mbali na walipitia vikwazo vingi sana hadi kufikia hapo walipo. Pengine itafika wakati ambapo inabidi umwambie tegemezi wako kuwa imetosha, aondoke ili akajifunze kujitegemea. Mara nyingi ujumbe kama huu huwa haupokelewi vizuri. Hapo ndipo huwa mwanzo wa kutokuelewana na ndugu. Visa na maneno kutoka kwa jamii huanza, huyu anasema hili, na yule anasema lile, ili mradi tu hali inakuwa ya kukoseshana amani. Wao wanachoona ni kuwa umemtendea vibaya ndugu yako kwa sababu umemfukuza. Kwa kawaida, huwa hawana muda wa kuangalia kwa undani wala kutafuta ama kuulizia sababu zilizopelekea ufanye hivyo, hata ufikie hatua ya kumfukuza ndugu yako. Kila mtu sasa ataziongelea habari zako ambazo sasa zitakuzwa kupindukia, kila mtu atasimuliwa. Wanaosikia habari hiyo watakuchukia sana na kukuona wewe ni mnyanyasaji. Sasa watu wataacha hata kutembeleana, urafiki, undugu utakwisha kwa sababu ambazo si za msingi.

Kutokana na akili ndogo ama kutojua, jamaa aliyefukuzwa na ndugu yake anashindwa kuelewa kuwa yale yaliyotokea ndio mtikisiko wake wa kumsogeza mbele kimaisha. Mtikiso huo alioupata utamfanya aamke na aanze kupambana na maisha kwa maendeleo yake ya bila utegemezi.

Yatupasa tukumbuke kuwa mambo mazuri yanakuja baada ya kutikiswa. Kuchukua ushauri ama kufuata maelekezo ni njia nzuri ya kujikwamua kimaisha. Tusione aibu kuchukua ushauri ama kufanya maamuzi magumu. Majaribu ni mtaji wa mafanikio. Ukijaribiwa usiogope kwani ni sehemu ya maisha na hivyo hayana budi kutokea. Bila mapito magumu, mara nyingi, mafanikio huwa ni ndoto.

The Healing Hands Project

The Healing Hands project will economically empower people to achieve financial autonomy by building entrepreneurial skills and embedding skills transfer within the community - eliminating poverty as a driver of ill mental health. Funds raised from the jewelry will help sustain the implementation of accessible psychosocial interventions in underserved communities and promote the economic empowerment of the grandmothers who have been trained in and are implementing WHO's mental health Gap Action Program. Healing Hands provides interpersonal counseling, group talk therapy, and psychoeducation resources delivered through arts, where clients learn to handcraft traditional beaded jewelry as a marketable skill. Follow us @TEWWYWisdom @WisdomWellnessCollection to stay up-to-date.

#MentalHealth #Grandmother #Wisdom #Wellness #mhGAP #HealingHands #Art #Culture #Tanzania

Previous
Previous

Eti Mtoto Wa Kike Ni Nyanya, Ikikaa Sana Itaoza

Next
Next

Jitihada Haiondoshi Kudra