Maisha Ni Mlima Na Mabonde

Alfreda George - Wisdom&Wellness Counselor (TEWWY)

Simulizi

by Alfreda George (Wisdom&Wellness Counselor - TEWWY).

Mwanadamu anapoishi hapa duniani angependa mambo yake yote yamwendee vizuri tu siku zote. Lakini kiukweli, hali haiko hivyo. Mara zote tunashindwa kukubaliana na hali tunayopitia. Mara nyingi tunaishia kulalamika tu, na kujiona kuwa hatufai au tuna bahati mbaya. Pale unapokuwa na watu waliofanikiwa kwa kuvuka viunzi, basi hapo ndio unazidi kunyong'onyea zaidi na hata kukata tamamaa kabisa.

Lakini yatupasa tukumbuke kuwa, katika kila jambo tunalopitia, limepangwa lipite kwako ili uweze kupanda mlima wako. Unachotakiwa kufanya, ni kujitahidi ushinde, la sivyo, ukishindwa, utakuwa unapiga kwata hapo hapo ulipo.

Hakuna jambo litakalokuja kwako bila kupitia magumu. Jambo gumu linapokufika, huo ndio unakuwa mlima wako au bonde lako. Cha msingi, inakupasa ufahamu kuwa maisha ni milima na mabonde, kuna kupanda na kushuka. Unatakiwa upambane ili uweze kuifikia siku yako, maana kila mtu ana siku yake ambayo anatakiwa aifikie. Haijalishi utachukua muda gani kuifikia hiyo siku, lakini, kumbuka, ipo siku nayo itakuja tu.

The Healing Hands Project

The Healing Hands empowers people to achieve financial autonomy by building entrepreneurial skills and embedding skills transfer within the community – alleviating poverty as a driver of ill mental health. Funds raised from the jewelry will help sustain free mental health services in underserved communities and promote the economic empowerment of trained grandmothers who implementing #WHO #mhGAP evidence-based psychosocial interventions. The project provides interpersonal counseling, group talk therapy, and psychoeducation resources, referrals, advocacy and awareness raising delivered through arts. Clients learn to handcraft traditional beaded jewelry as a marketable skill. Follow us @TEWWYWisdom @WisdomWellnessCollection

Previous
Previous

Tenda Wema Uende Zako, Usingoje Shukurani

Next
Next

Machozi Ni Nini?