MTEMBEZI HULA MIGUU YAKE

Suzan Njana
Wisdom&Wellness Counselor

Kigamboni, Dar-es-Salaam

Mtu mvivu mara nyingi ni mtembezi na anapenda kuishi kutegemea utembezi wake kula chakula atakachobahatika katika matembezi yake.Huyu ni mvivu,hana kazi maalumu na mtegemezi. Ndugu na jamii inayomjua humwita mtembezi hivyo hula miguu yake kwa kubahatisha chakula njiani kwa watu wanaomsaidia

Watu wa aina hii wanaweza kubadilika tabia ya uvivu na mtembezi kutokana na maonyo ya watu wanaoishi nao kwa kuwashutumu juu ya tabia hizo zinazowakosesha uhakika wa maisha.Taratibu baadhi yao hupunguza au kuacha na kuanza kushiriki kazi hadi kuwa na bidii katika zinazowaingizia kipato; hatimaye kubadilika na kuboresha hali zao za maisha.

Ushauri wa jamii inayowazunguka waathirika hawa huwa siyo rasmi.Maneno na matendo yao juu ya waathirika hutokea  kuwa fundisho kwao kwa kusikia,kuguswa,hadi kubadilika na kuwa watu wazuri.

Previous
Previous

KABLA HUJADANGANYWA NA WENZIO HUJAFA

Next
Next

MWENYE KISU KIKALI NDIO MLA NYAMA ILIYONONA