Usimtendee Mwenzako Usiyopenda Kutendewa

Usimtendee Mwenzako Usiyopenda Kutendewa

Msemo huu una maana kubwa. Katika maisha, kuna kufurahi kwa aina nyingi, hasa pale watu wanapokutana, wakaongea na kutaniana. Kuna bwana mmoja alipenda sana kuwatania wenzake. Naye siku moja wenzie nao wakamtania yeye. Bila kujua, kumbe ule utani ulikuwa karibia na ukweli wa yale yanayotokea nyumbani kwake. Ulikuwa unamgusa barabara.

Read More
Usiingilie Mazungumzo Ya Watu

Usiingilie Mazungumzo Ya Watu

Kuna watu katika maisha yao huwa wanapenda sana kuonekana wanaelewa sana habari nyingi za watu. Watu hao mara zote huwa wakiwakuta watu wako kwenye maongezi yao, lazima watajitahidi kuonyesha kuwa wanakijua hicho wanachoongea. Hapo hapo, huanza kuchangia bila hata ya kujua mazungumzo hayo yalianzia wapi. Tabia hii huwa siyo nzuri hata kidogo, inaweza kukuponza.

Read More
KUWA MAKINI, CHUNGUZA USHAURI UNAOPEWA KABLA YA MAAMUZl

KUWA MAKINI, CHUNGUZA USHAURI UNAOPEWA KABLA YA MAAMUZl

Gari ni aina ya chombo cha usafiri kinachoendeshwa kwa kutumia nishati ya mafuta na gesi. Dereva ndiye analiendesha na kulitunza gari. Endapo likipata hitilafu yeyote ile, dereva ndiye atakayelazimika kuteremka chini na kulikagua. Pale atakapogundua kama kuna hitilafu yoyote, ni wajibu wa dereva kutafuta mafundi wa kutatua tatizo hilo kwa kuwa wanayo maarifa ya kutosha.

Read More
Kuishi Kwingi Kuona Mengi

Kuishi Kwingi Kuona Mengi

Kuishi ni neno linalotokana na maisha. Maisha ni siku au miaka tunayojaliwa na Muumba wetu baada ya kuzaliwa. Wenzetu wa zamani waliishi miaka mingi sana, wengine miaka 700 mpaka 900. Nyakati hizi tulizo nazo kuishi kwingi ni miaka 100 tu tena ni kwa wachache sana. Kuishi kwingi na kuona mengi hapa anazungumziwa mtu aliyeishi miaka 50 au 60.

Read More
Fuata Maadili Uishi Kwa Amani

Fuata Maadili Uishi Kwa Amani

Amani ni kitu cha msingi sana katika maisha. Unaweza kuwa na kila kitu katika maisha yako lakini ukikosa amani moyoni mwako, yote yanakuwa ni kazi bure.

Read More
Tuwapende Ama Tuwachukie Watu Kwa Kadri

Tuwapende Ama Tuwachukie Watu Kwa Kadri

Kupendana ni jambo la heri na la kupendeza sana.Hata maandiko yanatuasa tupendane. Lakini inabidi tuwe makini katika hilo maana huyo huyo umpendae anaweza kukugeuka siku yoyote. Hapo unaweza hata kujutia ulichokuwa umemfanyia huko nyuma. Uzoefu pia unaonyesha kuwa unaweza ukamchukia sana mtu lakini baadaye akaja kuwa wa msaada sana kwako siku ukipata shida.

Read More
Duniani Kuna Watu Waliondaliwa Maisha Na Wanaojiandalia Maisha

Duniani Kuna Watu Waliondaliwa Maisha Na Wanaojiandalia Maisha

Msemo huu unazungumzia uhalisia wa maisha katika dunia hii tunayoishi. Wako watu wanaishi kutokana na hali ya wale waliowatangulia. Kama wazazi au walezi walikuwa na jina la kusifika, basi kizazi kinachofuata kitatembea katika hali ile ile. Kwa mantiki hii,?watakuwa wepesi kuonekana katika eneo lolote lile kutokana na majina makubwa wanayotembea nayo. Mfano kwenye siasa watoto wa wenye majina ni rahisi kufikiriwa na kupata kile wanachokitaka, pamoja na kazi nzuri, kisa tu, jina kubwa linawalinda. 

Read More