Penye Mafanikio Kuna Furaha

Penye Mafanikio Kuna Furaha

Shughuli yoyote ambayo mwanadamu anafanya ni kwa madhumuni ya kufanikiwa. Katika mafanikio hayo ndipo inazaliwa furaha. Daima ukiona mtu amefurahi sana, ukitafuta sababu utakuta kuwa kuna mahali amefanikiwa. Nyumba yeyote ambayo imejaa upendo, basi elewa kuwa pale pana mafanikio kwa njia moja au nyingine.

Read More
Heri Lawama Kuliko Fedheha

Heri Lawama Kuliko Fedheha

Lawama ni hali ya kulalamika kuhusu jambo ama tatizo fulani. Fedheha maana yake ni aibu. Mara nyingi watu hutumia muda wao mwingi kulalamikia ugumu wa maisha. Ukiwachunguza watu hao kwa undani utakuta ni wale ambao ni wavivu, wasiopenda kufanya kazi. Mara nyingi watu hao hushinda vijiweni na kuzungumza mambo ya umbea ambayo hayana tija kwao wala kwa jamii. Kati ya watu hawa huwa na dharau na kebehi, wasiotafuta fursa, wasiopenda kushirikiana na wenzao na wenye mtizamo hasi dhidi ya wenzao na wao wenyewe.

Read More
Mwongo Huwa Hasemi Yake

Mwongo Huwa Hasemi Yake

Mtu mwongo ni yule mtu ambaye anapenda kuongea mambo ya wenzake kwa ushabiki. Mara nyingi huwa anaongea katika mithili ya kumdhalilisha mtu. Watu wa aina hii huwa wana asili ya kuwa na marafiki wengi ambao huvutiwa na stori zake za uongo. Huo ni ubinadamu wa watu ambao hawajitambui. Mara nyingi, kinachofanyika hapo huwa ni unafiki mtupu.

Read More
Akufaaye Kwa Dhiki Ndiye Rafiki

Akufaaye Kwa Dhiki Ndiye Rafiki

Kulikuwa na bawana mmoja ambaye alitaka kujua rafiki yake wa kweli ni nani. Siku moja alimwambia mkewe, "Mke wangu andaa chakula kizuri na kingi. Nataka kula na rafiki zangu wapenzi". Mkewe alifanya kama alivyoamriwa na mumewe. Akanunua kila aina ya mapochopocho na kupika. Pia alinunua vinywaji vingi vya kutosha kwa ajili ya wageni wake.

Read More
Usiogope Kuchukiwa, Ogopa Kulaumiwa

Usiogope Kuchukiwa, Ogopa Kulaumiwa

Chuki na lawama ni mambo ambayo yanakuja kwa kasi sana katika maisha ya jamii zetu. Mbaya zaidi, katika mahali pa kazi, hayo yameanza kuwa ndio maisha ya wengi. Kwenye sehemu ya kazi, chuki huja kuhusiana na utendaji wa kazi wa mtu. Kuna ambaye anachukiwa tu kwa sababu ya utendaji wake wa kazi na umakini katika kuitenda kazi aliyokabidhiwa na mkuu wake wa kazi.

Read More
Adui Hatoki Mbali

Adui Hatoki Mbali

Usemi huu unatufundisha jinsi tunavyopaswa kuishi na jamii na marafiki wanaotuzunguka. Ni vizuri kuwa karibu na hao watu kwa sababu hata maandiko yamesema binadamu tupendane na tusaidiane. Tunapaswa kujua kuwa hayo yote tunatakiwa tuyafanye kwa kiasi na kwa makini sana. Kumbuka, wema wako unaweza kukupeleka kwenye kilio. Sio kilio cha kufiwa, bali tunaongelea kilio kitokanacho na matatizo utakayoyapata baada ya hapo. 

Read More
Njia Ya Mkato Tamu, Lakini Ina Madhara

Njia Ya Mkato Tamu, Lakini Ina Madhara

Mara nyingi kama mtu anataka afike haraka, anatafuta njia ya kukatisha, njia ya haraka. Njia hiyo inaweza kuwa nzuri pale tu utakapofanikiwa kufika kule uendako. Kuna wakati lakini njia ya mkato inaweza ikakupoteza na ukashindwa kufika uendako. Kuna baadhi ya binadamu, hupenda kutafuta mafanikio kwa kupitia njia ya udanganyifu, kama kutapeli wenzao. 

Read More
Tuwe Wastaarabu Na Busara Katika Maongezi

Tuwe Wastaarabu Na Busara Katika Maongezi

Binadamu tunatakiwa kuishi kwa kufuata taratibu fulani zilizopo kwenye jamii, hii ni pamoja na jinsi tunavyozungumza na wenzetu. Kwa maana hiyo, ukiwa mstaarabu na mwenye busara huwezi kuuliza uliza watu maswali ambayo hayastahili kuulizwa, maswali kama: ‘Bado hujaolewa tu?….Una watoto wangapi?…Utazaa lini?…Mbona umri umeenda?…na mengine mengi.

Read More