Tuwe Tayari Kufanya Kazi Wakati Wote
Kinachofuata ni kisa cha mama na mtoto wake wa kiume. Yaliyomo ndani ya kisa hiki yanaweza yakakuumiza sana kama una roho yenye huruma na ya kibinadamu
Nyoka Na Jongoo
Hapo zamani za kale, Nyoka alikuwa ana miguu lakini macho hakuwa nayo. Jongoo naye alikuwa na macho, lakini miguu alikuwa hana
Ukomo Wa Subira Yako Ndio Mwanzo Wa Husuda
Kila jambo linalofanywa na mtu yeyote lina mahali pa kuanzia. Katika kuanza jambo kunahitajika mipango thabiti ili liweze kutekelezeka. Utekelezaji wa mipango hiyo, utahusisha binadamu wengine kwa asilimia kubwa. Kwa kawaida, kipindi hicho huwa ni cha mpito
Wazazi Wana Haki Ya Kutunzwa Na Watoto Wao
Kinachofuata ni kisa cha mama na mtoto wake wa kiume. Yaliyomo ndani ya kisa hiki yanaweza yakakuumiza sana kama una roho yenye huruma na ya kibinadamu
Acha Kuishi Kwa Wasiwasi, Hapo Ulipo Bado Una Nafasi
Maisha ni kupanda na kushuka. Chochote utakachokifanya, ni lazima utapitia changamoto za aina mbali mbali. Changamoto hizo zisikufanye uishi kwa wasiwasi na pia zisikukatishe tamaa.
Tutumie Mikakati Thabithi Katika Kuwafunza Watoto Wetu Maadili Mema
Hapo zamani kulikuwa na kaka mmoja ambaye alikuwa akiwalea dada zake wawili. Aliwapenda sana na akawa karibu nao. Aliwalea vizuri na kuwapatia mahitaji yao ya msingi
Mtoto Umleavyo Ndivyo Akuavyo
Mithali hii ni ya msingi sana, kuanzia pale mtoto anapozaliwa kwani tabia ya mtu inaweza kuwa nzuri au mbaya kutegemea na alivyolelewa na kukuzwa. Mfano, kama baba anakuwa na tabia ya kufokafoka na ukali uliopitiliza kila anaporudi nyumbani, watoto wake huishi kwa kuogopa muda wao wote. Pia wanaweza wakajenga tabia ya kuwa na hofu kila wakati wanapomuona baba yao. Woga ukiwazidi pia huwafanya watoto kuwa na tabia ya uongo na hata ya unafiki. Watoto wana akili sana. Wanaweza wakaamua kuwa vile mzazi wanavyomuona anataka wawe
Mtandao Ni Uwanja Wa Ulaghai
Baadhi ya wasichana wamekuwa wakirubuniwa na baadhi ya wanaume wanaoishi nchi za nje. Warubuni na warubuniwa, hukutana kwenye mitandao ya kijamii. Utandawazi ndio chanzo kikubwa cha kuleta yote haya. Mahusiano huanzia hapo, kwenye mitandao, juu kwa juu
Fanya Kazi Vizuri Kwenye Nafasi Yako
Kazi ndio msingi wa maisha. Binadamu sote hujishughulisha na kazi ili waweze kuishi. Katika mchakato huo wa kufanya kazi, unakutana na watu wengi ambao nyote mpo kwa ajili ya kufanya kazi na kupata riziki
Kawia Ufike
Kukawia ni kuchelewa au kutofika kwa wakati unaotakiwa. Wanaposema kawia ufike wana maana chelewa lakini ufike mahali unapotakiwa kuwa. Msemo huu unatumiwa sana na baadhi ya watu wasiojitambua na wasiokuwa na uhakika wanatakiwa wafanye nini. Sehemu za ibada ni moja za sehemu ambazo watu hutumia sana msemo huu. Wanapoutumia msemo huu kwenye masuala ya nyumba za ibada, wanakuwa na maana kuwa hata wakikawia, ili mradi watakuwa wamefika, haijalishi sana. Kwa wanaosema hivi ina maana kuwa, cha muhimu kwao ni kuonekana kuwa walikuwepo ili mradi wasieleweke vibaya
Mwamini Mungu Si Mtovu
Alikuweko mtu mmoja na mkewe, hawakuwa na kitu, rasilimali yao kubwa ilikuwa ni kondoo na jogoo. Siku moja walipata habari kuwa rafiki yao alikuwa anakuja kuwatembelea. Mke alimwambia mume wake kuhusu ugeni huo. Alimkumhusha kwa kusema kuwa walikuwa hawana kitu chochote cha kumkirimu mgeni wao. Walichokuwa nacho ni huyo kondoo na jogoo. Lakini, mke aliongeza kuwa yeye asingependa kuwachinja wanyama wake, yaani kondoo jogoo
Kaa Mbali Na Mazoea
Maisha yetu katika ulimwengu huu ni ya vurugu kati ya mtu na mtu. Chochote mtu akifanyacho kimeanzia kwenye fikra zake. Kwa kawaida, mtu hawezi kukurupuka tu na kuanzisha kitu bila kufikiria na kupembua kama hilo jambo litawezekana ama la. Mara nyingi, tunafanya kosa kumshirikisha mtu ama watu mawazo yetu mapema mno. Inawezekana, huyo unayemshirikisha hawezi kukutia moyo ili ufanikiwe, binadamu wengi ndivyo walivyo. Wengi hupenda kukatisha tamaa wenzao na hata kunena maneno mengi ambayo yanaweza kukutoa kwenye wazo lako.
Fikra Zako Usimshirikishe Mtu
Maisha yetu katika ulimwengu huu ni ya vurugu kati ya mtu na mtu. Chochote mtu akifanyacho kimeanzia kwenye fikra zake. Kwa kawaida, mtu hawezi kukurupuka tu na kuanzisha kitu bila kufikiria na kupembua kama hilo jambo litawezekana ama la. Mara nyingi, tunafanya kosa kumshirikisha mtu ama watu mawazo yetu mapema mno. Inawezekana, huyo unayemshirikisha hawezi kukutia moyo ili ufanikiwe, binadamu wengi ndivyo walivyo. Wengi hupenda kukatisha tamaa wenzao na hata kunena maneno mengi ambayo yanaweza kukutoa kwenye wazo lako.
Elimu Bila Vitendo Ni Sawa Na Bure
Elimu ni maarifa anayopata mtu darasani. Vijana wengi wamepata elimu wakianzia chekechea hadi vyuo . Baadhi yao elimu hiyo imewasaidia, wakafanikiwa na wengine kwa bahati mbaya walishindwa
Binadamu Ana Nyuso Mbili, Kaa Nae Kwa Akili
Mara nyingi tumeona kuwa siyo watu wote wanaokuzunguka ni wema kwako. Wewe unaweza ukajiona kuwa ni mwema kwa watu na wao , vivyo hivyo, ukawaona ni wema kwako. Katika imani hiyo unaweza ukajiridhisha na kuona kuwa una ndugu au marafiki wa haja, marafiki wa kukimbiliwa ukiwa na shida.
Kisa Cha Kuku Na Kanga
Hapo zamani kuku walikuwa ndege wa mwituni. Waliishi pamoja na kanga na ndege wengine. Basi siku moja ikaja mvua kubwa huko mwituni. Kanga akamwambia kuku, nenda kwa binadamu ukaombe moto ili tuje tuote. Baridi imezidi, ni kali sana. Kuku alitii agizo la kanga. Alienda, na alipofika kwa binadamu, alikaribishwa vizuri. Binadamu alimuuliza shida iliyompeleka hapo.