Kisa Cha Kuku Na Kanga

Kisa Cha Kuku Na Kanga

Hapo zamani kuku walikuwa ndege wa mwituni. Waliishi pamoja na kanga na ndege wengine. Basi siku moja ikaja mvua kubwa huko mwituni. Kanga akamwambia kuku, nenda kwa binadamu ukaombe moto ili tuje tuote. Baridi imezidi, ni kali sana. Kuku alitii agizo la kanga. Alienda, na alipofika kwa binadamu, alikaribishwa vizuri. Binadamu alimuuliza shida iliyompeleka hapo.

Read More