Nyani Akiumwa Ukimpa Dawa Akipona, Jiandae Mahindi Yako Kuliwa
Kuna ndugu anaweza kuja kwako akiwa hoi kimaisha, hata hela ya kula hana. Safari yake ni kuja kuomba msaada. Unampokea na kukaa naye nyumbani kwako. Anakula kile ambacho Mungu amekujalia hapo nyumbani pako.
Furaha Ni Kama Marashi Kwani Huongeza Maisha
Wahenga wa kale walisema, "Kitu furaha ni sawasawa na marashi”, kwani huwezi kujipulizia wengine wasisikie harufu yake. Hii inajidhihirisha wazi kwamba ukiwa na furaha huwezi kuificha kwani mtu yeyote atakayekuona atatambua kuwa umefurahi au una furaha. Basi, endapo wewe umefurahi, jitahidi na watu wengine nao wafurahi kutokana na furaha yako.
Usitegemee Uzuri Wako Maana Kuna Siku Utazeeka
Wako mabinti zetu wengi ambao wanajiona ni wazuri kwa umbo na sura. Watu hao mara nyingi hujiona kuwa ni bora zaidi kuliko wengine. Na huwa wanapenda hata kuchagua ni nani watakuwa wenzi wao.
Anayekukosoa, Anakujenga!
Ni kawaida ya watu wengi kupenda kuonekana kuwa wako mbele sana katika kila jambo wanalolifanya. Hakuna mtu anayetaka kuonekana kuwa hawezi.
Mpe Adui Yako Tabasamu Badala Ya Machozi
Unaporuhusu uchungu na maumivu ndani yako ni rahisi sana kuchoka na kukataa tamaa. Usibebe kila kitu, na wala usichukulie kila kitu kwa uzito, utaelemewa.
Kubali Kupoteza Ili Uende Viwango Vingine
Katika maisha unaweza kupoteza nafasi, au watu uliowaamini sana. Pengine hata uliweza kufikiri kuwa bila wao maisha au malengo yako hayatafanikiwa.
Maisha Ni Kutegemeana
Maisha ya mtu ni fumbo zito. Kila mtu ana umuhimu katika maisha ya mwenzake. Hii ni kwa sababu maisha ni kutegemeana.
Wakati Mwingine Hawakupendi, Wanakupenda Kwa Kile Ulicho Nacho
Ni ukweli usiopingika kuwa watu humpenda mtu mwenye nacho. Watu wa aina hii, yaani wale wenye nacho, huwa na marafiki wengi kupita maelezo. Ukweli huu huonekana zaidi kama huyo mtu atakuwa ni mtoaji sana na ambaye anapenda kusaidia watu.
Heri Shetani Unayemjua, Kuliko Malaika Usiyemjua
Tupo duniani tukizungukwa na watu mbalimbali na wenye tabia tofauti tofauti. Tunaishi kwa kutegemeana maana sisi ni wanadamu ndiyo maana utaona watu wanasaidina kwa shida na raha. Zaidi ya hapo utaona kwenye jamii zetu, kuna watu wanaishi kwa kupendana kama ndugu na kufanya vitu pamoja na kushauriana kwa kila jambo linalokuja mbele zao.
Jielewe Kwanza Mwenyewe, Watakuelewa Pia
Kama unataka kuwa kitabu cha kusomwa hata na vizazi vijavyo, hakikisha unajisoma na kujielewa mwenyewe, kwanza kwa mawazo yako na ujumbe wako. Ila kama unataka kuwa kitabu cha kusomwa leo na baadae kusahauliwa, basi endelea kutafuta kueleweka na watu wa leo.
Usitumie Usomi Wako Kuwanyanyasa Na Kuwatambia Wenzako
Wako watu wanaojiona, wanaojitapa na kutamba kuwa wana akili sana. Hujiona wamesoma na wameelimika zaidi ya wengine. Watu hawa huchukua fursa hiyo ya kuelimika kama fimbo ya kuwachapia wenzao. Huwanyanyasa wenzao kwani huwaona kuwa ni wajinga na pia hawana elimu. Hali kadhalika, huwadharau, kiasi kwamba hata kuongea nao inakuwa ni shida, kisa, eti hawajasoma.
Mpatie Mtu Ujira Wake Kwa Wakati Anaostahili
Kuna aina nyingi za ajira hapa duniani. Usemi huu unawalenga wale tunaowaajiri hasa kwenye kazi za nyumbani (house girls). Kuna tabia mbaya ya baadhi ya waajiri kwenye sekta hii kutokuwajali na kuwathamini wafanya kazi wa sekta hii.
Yatima Hadeki
Neno yatima au ukiambiwa yule ni yatima kila mtu ataelewa. Yatima ni mtoto ambaye, aidha kafiwa na mzazi mmoja au kafiwa na wazazi wake wote wawili.
Usimtekenye Aliyekubeba, Atakudondosha
Maisha yetu ni ya kutegemeana kwa kiwango kikubwa sana. Hakuna mtu atakayesema hapa alipo amefika kwa juhudi zake mwenyewe. Lazima kuna mahali alifika akakwama, na mtu mwingine akamkwamua na hatimaye akatoka.
Barua Ya Moyo Husomwa Kwenye Paji La Uso
Moyo ni kitu kidogo sana katika mwili wa mwanadamu. Moyo huwa hauonekani kwa jicho la kawaida, lakini moyo ndio uhai wa mtu ulipo.
Cha Mtu Mavi
Tunaishi duniani kwa viwango tofauti vya maisha. Kuna baadhi ya watu wanavyo vitu vya kupitiliza, hadi inakuwa kama kufuru. Wengine wanavyo vya wastani, na wengine wanavyo kidogo au hawana kabisa. Kutokana na hali hiyo wanadamu tunaishi kwa kutoridhika na hivyo tulivyo navyo.
Thamani Ya Mbwa Huisha Mwisho Wa Mawindo
Ni ukweli usiopingika kuwa katika maisha thamani ya mtu huisha pale anapokuwa hayuko tayari tena ama hana uwezo wa kuendelea kutoa msaada. Hii inaweza kutokea kutokana na hali yake kiuchumi kupungua au kutetereka.
Tuache Ukatili Kwa Wanyama, Malipo Ni Hapa Hapa Duniani
Palikuwa na kijana mmoja ambaye alirithi mifugo kutoka kwa baba yake. Hivyo alikuwa mfugaji na mchungaji. Miongoni mwa mifugo aliyorithi, walikuwepo punda, ng'ombe, mbuzi, kondoo, mbwa na kadhalika. Akiwa machungani alikuwa na tabia mbaya ya kuitesa baadhi ya mifugo yake. Moja kati ya wanyama aliyekuwa anateswa sana ni punda ambaye alikuwa anamsadia kubeba mizigo.
Mfungwa Hachagui Gereza
Huo msemo niliujumuisha na usemi ambao tumezoea kuuzungumza. Msemo huo ni ule wa: 'Sheria ni msumeno ambao unakata kote kote'. Nilishuhudia tukio hili nilipokuwa nasafiri toka Mwanza kuja Dar. Tulipofika Shinyanga tuliona abiria watatu wameingia kwenye basi tulilokuwemo. Mmoja wa abiria hao alikuwa amefungwa pingu.
Tuchukue Tahadhari Stahiki, Dunia Inabadilika Kwa Kasi Mno
Ni ukweli usiopingika kuwa dunia inabadilika kwa kasi kubwa sana kila kukicha, mithili ya mtu aliyegeuza miguu juu, kichwa chini. Dunia ya leo siyo kama ile ya zamani. Dunia ya sasa imekuwa na mambo mengi ya aibu, maovu ya kutisha na ya kusikitisha kiasi kwamba ubinadamu au utu umetoweka. Imefika mahali hatuna huruma tena, tumekuwa kama wanyama. Mambo mengi mabaya yanaibuka kila siku na hata usalama wa binadamu upo mashakani.