Jifunze Kujishusha Machoni Pa Watu Wengine

Jifunze Kujishusha Machoni Pa Watu Wengine

Baadhi ya watu wana ile tabia ya kuona kwamba wao ndio pekee wa kuweza kutoa maamuzi ya aina yoyote wakiwa kwenye kundi la watu. Tabia ya watu hawa ni ya kujiona na kujisikia kuwa wao ni bora kuliko watu wengine. Watu hawa hufikia hatua ya kuchukia pale wanapotoa jambo/ushauri mbele za watu na halafu usikubaliwe. Huwa hawaelewi kabisa kwa nini yale wanayosema yasikubaliwe na watu. 

Read More
Ujana ni Dhahabu

Ujana ni Dhahabu

Katika maisha tunaweza kusema kuwa, "umri wa ujana" ni kipindi cha dhahabu ambacho tunatengeneza marafiki wengi na kupoteza wengi pia. Katika kipindi hiki, uamuzi wa kuyaharibu au kuyatengeneza maisha yako ili yawe mazuri baadaye unao wewe mwenyewe. Kwa hiyo inakupasa kukumbuka kuwa kipindi hiki kikishapita hakijirudii tena. Hivyo kitumie vizuri uwezavyo.

Read More

Usitoe Maamuzi Wakati Una Hasira

Hasira ni ile hali ya kuhamaki kwa jambo ambalo umesikia au umefanyiwa na mtu bila kukubaliana ama kuridhika nalo. Inawezekana likawa ni jambo la kusingiziwa au la. Hasira inaweza kukupelekea kuamua chochote kibaya, ukafikia hata hatua ya kuua. Mara nyingi hasira inaishia kwenye kujuta kwa lile ulilolifanya kwa kukusudia ama kutokusudia. Sambamba na usemi huu ni ule wa Majuto ni Mjukuu. Tunaaswa kutokuamua jambo lolote wakati tuna hasira.

Read More
Mgeni Njoo, Mwenyeji Apone

Mgeni Njoo, Mwenyeji Apone

Mgeni ni mtu anayekuja kwenye makazi ambayo hana mazoea nayo au ni mahali ambapo siyo kwake. Kwa kawaida, mtu huyu anapokuja humfanya mwenyeji wake kuhangaika kutafuta hiki na kile, ili mradi yeye na mgeni wake waweze kufurahi pamoja. Mgeni huyo anaweza kuwa ni ndugu ambaye ametoka mbali kuja kusalimia tu ama kwa shughuli nyingine.

Read More
Ni Rahisi Kubeba Kikombe Kisicho na Kitu Kuliko Kile Chenye Kitu

Ni Rahisi Kubeba Kikombe Kisicho na Kitu Kuliko Kile Chenye Kitu

Kwenye maisha ya binadamu, tunaposema “Ni rahisi kubeba kikombe kisicho na kitu kuliko kikombe chenye kitu“, ina maana kubwa. Kwa mfano, ukiishi na watu mbalimbali huku ukijivuna, ukiwadharau na kuwaona hawafai, hawajui kitu, ila wewe unajihesabia kuwa ndiye unayejua kila kitu, watu watakulinganisha au watakufananisha na kikombe kisicho na kitu chochote ndani yake, yaani kikombe kitupu.

Read More