Hasara Haiogopi Mtaji

Hasara Haiogopi Mtaji

Mtaji ni nyenzo ambayo inatumika kwa ajili ya kutengeneza jambo fulani lenye tija ndani yake. Inawezekana ikawa ni fedha au kitu kingine ili mradi kiweze kuleta tija. Mtaji unatakiwa uzalishe na utoe faida. Ili iweze kuwa hivyo, unahitajika umakini wa hali ya juu endapo utataka kufikia malengo uliyojipangia.

Read More
Muongo Huwa Haulizwi

Muongo Huwa Haulizwi

Hapa duniani kuna watu wa aina mbalimbali. Ndio maana watu husema dunia ni uwanja wa fujo. Kuna makundi mengi yenye huluka tofauti tofauti. Katika makundi hayo liko kundi moja ambalo ni gumu sana nalo ni lile kundi la waongo au wazushi. Kazi kubwa ya kundi hili huwa ni kuvuruga jamii. Watu walioko kwenye kundi hili ni wa hatari sana. Wao ni mabingwa sana wa kuleta uchonganishi na kugonganisha watu ili wasielewane. Pale wanapoona fulani na fulani wanaelewana, wao hukosa raha. Lazima watatafuta njia ama namna ya kuwavuruga. Watajitahidi kutunga uongo unaoendana na ukweli ili mradi tu waweze kuwatenganisha.

Read More
Mazoea Kutwaa, Kutoa Ni Vita

Mazoea Kutwaa, Kutoa Ni Vita

Kuna watu ambao wamejijengea tabia ya kupokea tu kutoka kwa wenzao, lakini wao sio wepesi wa kutoa kabisa. Watu wa namna hii, kupokea kwao huwa ni rahisi, lakini inapofika kwa wao kutoa, wanakuwa hawako tayari kabisa kufanya hivyo. Ukweli ni kwamba hata huwa hawakumbuki kurudisha fadhila walizotendewa na wengine.

Read More
Hasira Hasara

Hasira Hasara

Mara nyingi katika maisha yetu, baadhi ya watu huwa sio wavumilivu pindi pale wnapopa taarifa mbaya. Jambo linapowafikia wanashindwa kufanya uchunguzi kwanza ili kupata ukweli. Wengi huwa wana maamuzi ya haraka, hali ambayo inaweza kuwafanya watende mambo yasiyopendeza kwenye jamii. Matokeo yake ni vurugu na magomvi na kuweka vikao vya kusutana. Hali hii huweza kusababisha watu kuwa na mahusiano mabaya na hata kununiana bila uhakika wa jambo lenyewe.

Read More
Heri Kuaminiwa Kuliko Kupendwa

Heri Kuaminiwa Kuliko Kupendwa

Siku zote, binadamu huwa tunataka kupendwa, na si vinginevyo. Huo ni ubinadamu kabisa, hakuna cha ajabu hapo. Mtu anakuwa na furaha pale anapogundua kuwa watu wanamfurahia na kumpa sifa nyingi za kumfanya aonekane ni mtu muhimu katika jamii. Lakini ni lazima tukumbuke kuwa inawezekana hao wanaokumwagia sifa wana sababu zao. Pengine ni unafiki tu na huenda kuna jambo wanalolitaka kutoka kwako. Furaha yako isiwe ya kukurupuka tu, yakupasa utafakari kwanza. Huenda mtu huyo ana jambo ambalo anataka asaidiwe katika eneo fulani linalomsumbua. Anajua kuwa ataweza kusaidiwa pale atakapokumwagia sifa lukuki.

Read More
Hakuna Anayefika Juu Kwa Kulala Usingizi

Hakuna Anayefika Juu Kwa Kulala Usingizi

Yatupasa tujue kuwa tukipenda usingizi hatutafika popote kimaendeleo. Hiyo huwa ni dalili tosha ya kuukaribisha umaskini. Tumeshuhudia wenyewe katika maisha yetu ya kila siku. Watu wengi wenye juhudi ya kufanya kazi kwa bidii wana maisha mazuri. Wana uwezo wa kusomesha watoto wao, uwezo wa kula vizuri, hali kadhalika, uwezo wa kuwa na nyumba nzuri za kuishi.

Read More
Ndoa Ina Furaha, Na Maumivu Pia

Ndoa Ina Furaha, Na Maumivu Pia

Kwa kawaida kila mtu anategemea maisha ya ndoa kuwa ya furaha, lakini wakati mwingine yanaweza kuwa ni kinyume chake. Matatizo yanapoanza, matokeo makubwa ya hisia hasi, mathalani uchungu, hofu, moyo kujeruhika, wasiwasi, na hata msongo wa mawazo hujitokeza. Aidha, hisia hasi huweza kuzalisha chuki zaidi, hasira, ugomvi endelevu, usaliti, kununiana,na mawasiliano mabaya ndani ya nyumba.

Read More
Cha Ndugu Hakiwezi Kua Chako, Kiogope

Cha Ndugu Hakiwezi Kua Chako, Kiogope

Watu wengi hupenda sana kujisifu kutokana na kile alicho nacho ndugu yake. Ni ukweli usiopingika kuwa mtu yeyote hatakiwi kujisifu kwa ajili ya mali ya ndugu yake. Hii ni kutokana na ukweli kuwa vitu hivyo au mali hizo siyo za kwake. Kila mtu yampasa atafute kilicho chake. Kitu kikiwa cha kwako unakuwa na uhuru nacho na unaweza ukafanya nacho chochote unachotaka.

Read More