Chui Hakumbatiwi

Chui Hakumbatiwi

Fikira za mwanadamu huwa hazina ukomo. Hii ni kutokana na ukweli kwamba binadamu ana mambo mengi ya kuwaza wakati wote. Kuna mambo tunayawaza yakiwa ni ya hatari kwetu na ya kuhuzunisha pia. Mambo ya kuhuzunisha huwezi kuyakumbatia. Mambo hayo ni kama uvivu, wizi, kutowajibika, kusengenya na kusema uongo. Ukitaka kuwa na amani, inakupasa ujitenge na mambo hayo, hii ni kwa ajili ya ustawi wako mwenyewe.

Read More
Jipe Muda Wa Kufurahia Yale Uliyobarikiwa

Jipe Muda Wa Kufurahia Yale Uliyobarikiwa

Ni jambo la kawaida kabisa kwa binadamu kupenda kuwa na furaha siku zote za maisha yake. Lakini yatupasa tuelewe kuwa furaha hiyo haipatikani ki urahisi. Inakupasa kuhangaika na kujishugulisha ili uweze kutimiza matakwa yako na ufurahie matunda ya kazi zako. Lakini badala ya kujishughulisha, inafikia wakati tunaangalia fulani kafanya hiki au kile na ndio maana kafanikiwa zaidi. Tunafikiria kuwa mafanikio yake huenda yalipatikana kiurahisi. Hatuchukui muda kuchunguza alikotoka hadi akafikia hapo alipo. Tunafikiri yote aliyonayo aliyapata kiurahisi tu.

Read More

Mafanikio Ya Mtu Hutegemea Uwezo Wa Kufikiri Na Kutafakari

Mafanikio ya mtu yeyote hapa duniani hutokana na bidii, kujiamini, kiwango na uwezo wake wa kufikiri na kutafakari. Aidha, wengine hupoteza muda wao kuwaza jinsi watu wengine wanavyowaona, wanavyowafikiria, wanavyowatafakari na wanayowawazia.Hata hivyo inabidi kujua kwamba, ili uweze kufanikiwa katika maisha, kamwe usitumie muda wako kuwaza kuwa nikifanya hivi wengine watanionaje ama watanifikiriaje. Inakubidi wewe ufanye shughuli zako kwa kujiamini. Ili mradi unachofanya kiwe ni sahihi mbele ya Mungu na mbele za binadamu wenzio.Kwa kuwa na mtizamo huo chanya, mawazo ya watu wengine hayataruhusiwa kuitawala akili yako. Mtazamo chanya utakufanya usimame imara kwenye kile unachokiamini na hatimaye, utapata mafanikio.Hapa tunapata funzo kuwa, kamwe tusiumize vichwa vyetu na kuchukua muda mwingi kuwafikiria watu wengine wanachowaza juu yetu. Jiulize wewe unawaza nini kuhusu wao pamoja na kwamba hata wewe siyo kazi yako kuwawazia wengine. Wewe jali kazi na maisha yako na mambo yanayokuhusu. Acha kuwafikiria wao kwani mambo yao wewe hayakuhusu.

Read More
Debe Tupu Haliachi Kutika

Debe Tupu Haliachi Kutika

Tupo katika ulimwengu wenye mambo mengi yanayotuzuguka. Kwa kawaida, maisha yetu yako katika makundi makundi. Yapo makundi yenye uwezo mkubwa, yapo yale yenye uwezo wa kati, hali kadhalika yale ya kawaida. Kundi hili la mwisho ni lile ambalo inawezekana hata riziki ya siku ni ya kubabaisha. Inaweza hata siku ikapita bila ya kuwa na chochote. 

Read More