Mwenye Shoka Hakosi Kuni

Mwenye Shoka Hakosi Kuni

Kuna watu ambao wamejijengea tabia ya kupokea tu kutoka kwa wenzao, lakini wao sio wepesi wa kutoa kabisa. Watu wa namna hii, kupokea kwao huwa ni rahisi, lakini inapofika kwa wao kutoa, wanakuwa hawako tayari kabisa kufanya hivyo. Ukweli ni kwamba hata huwa hawakumbuki kurudisha fadhila walizotendewa na wengine.

Read More
Lawama Ni Kama Moshi

Lawama Ni Kama Moshi

Katika mikusanyiko mingi ya watu, kuna mambo mengi ambayo hutokea. Kuna misuguano ambayo nayo hutokea kati ya mtu na mtu au kikundi na kikundi. Kulaumiana huwa ni kwingi sana kwa sababu kila mtu hujiona ana haki ya kusema chochote alichokuwa nacho, kiwe cha kweli au cha uongo.

Read More
Mzoea Kutwaa, Kutoa Ni Vita

Mzoea Kutwaa, Kutoa Ni Vita

Kuna watu ambao wamejijengea tabia ya kupokea tu kutoka kwa wenzao, lakini wao sio wepesi wa kutoa kabisa. Watu wa namna hii, kupokea kwao huwa ni rahisi, lakini inapofika kwa wao kutoa, wanakuwa hawako tayari kabisa kufanya hivyo. Ukweli ni kwamba hata huwa hawakumbuki kurudisha fadhila walizotendewa na wengine.

Read More
Ni Rahisi Kusikia Maneno ya Mdomoni Kuliko Ya Moyoni

Ni Rahisi Kusikia Maneno ya Mdomoni Kuliko Ya Moyoni

Kilichopo ndani ya moyo wa mtu ni vigumu sana kukijua hata kama ni ndugu yako au rafiki yako. Waswahili walisema, moyo wa mtu ni msitu mnene ambao unatoa maamuzi yaliyo sahihi au magumu. Yawezekana kabisa jambo ambalo litaamuliwa na moyo likakinzana na fikra ya mtu lakini kwa sababu moyo hauna mshauri basi maamuzi yanaweza kuwa ni mabaya. Ubaya wake utaonekana baadae wakati ambao inakuwa vigumu kubadilisha.

Read More
Rafiki Wa Kwali Ni Yule Anayefahamu Matatizo Yako Na Bado Uko Naye

Rafiki Wa Kwali Ni Yule Anayefahamu Matatizo Yako Na Bado Uko Naye

MAZUNGUMZO YA BUSARARAFKI WA KWELI NI YULE ANAYEFAHAMU MATATIZO YAKO NA BADO UKO NAYEALFREDA GEORGEHapa duniani tuna makundi mengi ambayo tunaishi nayo siku hadi siku. Makundi hayo yamegawanyika kutokana na hali halisi ya maisha. Kuna kundi la familia, ndugu, marafiki, na pia wale unaofanya nao kazi. Kundi hili la mwisho, kazi ndio inakuwa kiunganishi kikubwa..Kundi la marafiki huwa ni kubwa zaidi. Kundi hilo linaweza kuwa ni zuri au la kinafiki . Kuna rafiki ambaye anakuwa ni kama ndugu unaweza usimtofautishe na ndugu wa familia yako. Rafiki unaweza ukamuamini kiasi kwamba kila jambo lako utamshirikisha, liwe baya au zuri.Katika marafiki inabidi uangalie yule ambaye anaweza kubeba siri zako na kwamba kama umemshirikirsha, basi usije ukazisikia sehemu yoyote. Hapo unahitaji umakini wa kufahamu mtu aliye sahihi. Ukikosea basi utaangukia pabaya.Umakini wako utakupa rafiki mzuri na wa kweli. Rafiki huyo huwa yuko tayari kubeba matatizo yako pindi yanapotokea. Mwingine anaweza akakuacha njia panda ukihangaika peke yako. Rafiki wa aina hiyo sio rafiki mzuri .Rafiki mzuri na wa kweli, ni yule anayekufaa wakati wa shida. Ni yule anayeona tatizo lako kama la kwake the na anakuwa tayari kukutetea kwa hali na mali, kwenye jambo dogo ama kubwa, kuwe na mvua ama jua, yeye anakuwa mstari wa mbele kukusaidia wakati wowote na kwa hali yoyote, ili mradi wewe upate msaada unaouhitaji kwa wakati muafaka. Marafiki wa namna hii kwa hakika si wengi, ni wachache mno. Ukiwa nao, yakupasa umshukuru Mungu, na uwasike vizuri, usiwaachilie.

Read More
Uwe Mkweli Na Mwenye Maamuzi Sahihi

Uwe Mkweli Na Mwenye Maamuzi Sahihi

Kuna mambo ambayo unatakiwa kuzingatia katika maisha yako. Mojawapo ya mambo haya ni kufanya maamuzi sahihi. Ukweli unaonyesha kuwa maskini walio wengi na watu ambao wameshindwa kuendesha biashara ama waliokwama kwenda mbele, ni wale ambao wana tabia ya kushikilia mambo ya jana. Ukweli ni kwamba, jana ilikwishapita na hivyo haiwezi kukupa chochote.

Read More