
Kipimo Chako Siku Zote Ni Ufanisi.
Binadamu wote tumeumbwa tofauti katika nyanja nyingi. Wengi huwa wana ile hali ya kutaka kueleweka au kutambulika hata kama hawana jambo la maana walifanyalo. Kama ule usemi wa debe tupu haliachi kutika ndivyo ilivyo kwa wengi katika jamii zetu.

Mafanikio Ni Mchakato!
Kwa kawaida binadamu huwezi kuhesabu mafanikio yako ukiwa umekaa au umebweteka tu. Kama ilivyo kawaida, siku huwa zinabadilika na kila siku ina mambo yake, na mafanikio vivyo hivyo. Lazima upitie mchakato ili uweze kufanikiwa. Endapo mchakato utaonyesha kukukwamishia mafanikio yako, basi elewa huo sio mchakato sahihi. Cha msingi, usikate tamaa endelea kuangalia mchakato mwingine. Unaweza hata kumshirikisha mtu ambaye unamuamini ambaye anaweza akakusaidia kwa mawazo au hata kwa mtaji.

Elewa Kusudi La Kuwepo Kwako!
Uwepo wa kila mtu unakuwepo tokea mtu akiwa tumboni mwa mama yake. Hivyo ulivyo sasa ni kusudi ambalo ulizaliwa nalo. Kutokana na hali hiyo unatakiwa kujua kusudi lako ili uweze kupanga namna ya kupata mafanikio.

Kaa Mbali Na Wenye Fikra Hasi, Kwao Hakuna Jema!
Watu wenye fikra hasi ni wale wanaopenda kukatisha tamaa wenzao kwa kila wanalolitenda. Wao kazi yao ni kukandamiza tu wenzao na pia ni kujaribu kwa kila hali kufuta maono ama ndoto za wenzao.

Huwezi Kupata Kivuli Kwenye Mti Uliopinda!
Mti ni nishati ambayo ina matumizi mengi sana. Kwenye mti tunapata matunda, tunapata mbao, kuni na hata dawa. Wengine hupanda miti kwa ajili ya kivuli, hususan kwenye maeneo ya kuzunguka makazi yao.
Usitengeneze Kundi La Kumchukia Mtu Kwa Chuki Zako Binafsi!
Ulimwengu huu umejaa shida na vurugu tele kila uchwao. Karibia kila siku tunakutana na mambo mengi mazuri na mabaya pia. Mambo yaliyomabaya hutokana na mahusiano katika jamii nyingi. Migongano ya mtu na mtu au kikundi na kikundi, ni mambo ya kawaida katika maisha tunayoyapitia.

Mtenda Wema Ana Malipo!
Hapa duniani yako mambo mengi sana tusiyoyajua. Lakini ili tufanikiwe katika jambo fulani lazima tuwe na ufahamu na hilo jambo.

Usihukumu Kitabu Kwa Ganda La Juu.
Katika maisha yetu sisi binadamu tuna mambo ya kudharauliana sana. Hiyo inakuja kwa sababu ya kutokumuelewa mtu kwa undani wake. Inatokea pengine mtu kwa kukuangalia tu anakutafsiri kwa jinsi anavyokudhania yeye.

Uvivu Ni Adui Wa Mafanikio
Uvivu ni kizuizi kikuu cha mafanikio yabinadamu yeyote. Hata maandiko matakatifu yanadhihirisha hayo kwa kusema kuwa mvivu siku zote hufa maskini na hatakiwi kupewa chakula. Tunaambiwa kuwa mwenye bidii hula jasho lake ambalo ni bidii yake mwenyewe na hufa akiwa tajiri.

Mkataa Kwao Mtumwa
Msemo huu unaweza ukamaamisha mtu anayekataa kabila lake, anayekataa utaifa wake na akaweza kuwakataa hata wazazi na ndugu zake pia.

Mpanda Hovyo Hula Hovyo.
Neno mpanda linatokana na neno kupanda. Mpanda ovyo ni yule mtu anayepanda vibaya bila mpangilio. Mtu huyu hupanda bila kufuata hatua zitakiwazo. Mathalani, wakati wa kupanda inatakiwa kuzingatia nafasi kati ya mbegu na mbegu, hali kadhalika, kati ya mstari hadi mstari. Pia inabidi kuzingatia ubora wa mbegu zenyewe ili kupata mavuno yaliyo mengi na bora. La sivyo, kinyume na hapo, mavuno yatakuwa kidogo na yenye ubora duni. Pale mavuno yanapokuwa duni hayatakidhi kuliwa kwa mwaka mzima uliotegewa. Ndio maana ya usemi huu kuwa aliyepanda ovyo, atakula kwa miezi michache tu, kinyume na mategemeo yake.

Nazi Haishindani Na Jiwe!
Nazi ni tunda linalotokana na mti wa mnazi. Kwa kawaida, nazi ni ngumu na jiwe ni kipande kinachotokana na mwamba. Ndio maana tunasema, nazi haiwezi kushindana na jiwe kamwe, kutokana na uimara wa jiwe.

Avuae Nguo Huchutama.
Neno avuae ni kisifa kinachotokana na tendo la kuvua nguo. Msemo huu unamaanisha avuae ni tendo la kuvua nguo na kubaki utupu. Kuchutama ni kuinama kwa ajili ya kuficha utupu.

Akiba Haiozi
Ndege ni viumbe hai na wana mabawa na wana miguu miwili. Wana uwezo wa kuruka. Chakula chao ni wadudu na nafaka.

Anachoweza Kukufanyia Jogoo Ni Kukupigia Kelele Na Sio Kukutoa Kitandani.
Maisha yetu yanatawaliwa na mambo mengi sana. Mengi tuyafanyayo yanatokana na kufundishwa au kuelekezwa. Katika mambo mengi tunayofundishwa kama tungekuwa tunayatendea kazi tungekuwa mbali sana. Kumbuka kuna mangapi tumesoma ambayo ni ya msingi lakini hatuyafanyii kazi. Huu ndio ukweli wenyewe.

Ukiambiwa Ubaya Wa Mtu, Tafuta Uzuri Wake.
Binadamu tuna tabia moja ya ajabu sana. Mara nyingi tukiambiwa kuwa fulani ni mbaya tunaamini mia kwa mia na kuufanya ubaya wake kuwa ni fimbo ya kumchapia kila uchao. Kila jambo atakalotenda linakuwa ni baya tu kwa jamii inayomzunguka. Ubaya wake unakuwa umekwisha tia mhuri kwenye mioyo ya watu kiasi kwamba hata akipita mahali popote pale atakuwa ni wa kunyooshea vidole tu.

Mafanikio Yanahitaji Kufahamu Na Kukipenda Kile Unachokifanya.
Hapa duniani yako mambo mengi sana tusiyoyajua. Lakini ili tufanikiwe katika jambo fulani lazima tuwe na ufahamu na hilo jambo.

Usiige Wala Kukata Tamaa Ungali Hai.
Mara nyingi sisi,binadamu tunakuwa na tabia ya kukata tamaa ya kuendelea na maisha mara tunapokwama kidogo. Huwa tunasahau kuwa mafanikio hayaji ghafla na kwamba nyuma ya kila fanikio, lazima kuna maumivu makali.

Donda La Kichwa Mkaguzi Mkono!
Ni ukweli usiopingika kuwa kila binadamu lazima atakuwa na mtu au watu wa karibu ambao huwa ni tegemeo lake katika mambo mengi ayatendayo, hususani wakati wa shida ama wakati wa raha. Wako watu ambao wanaweza kuwa karibu zaidi kiasi kwamba kunakuwa hakuna jambo unalowezakulifanya bila wao kujua au kuchangia mawazo.

Wajibika Na Maisha Yako
Hapa duniani, kila mtu anatakiwa kupambania maisha yake. Unaposimamia na kudhibiti shughuli zako mwenyewe utaridhika, utapata amani, furaha na faida.