Jembe Halimtupi Mkulima!

Jembe Halimtupi Mkulima!

Jembe ni nyenzo inayotumika na mkulima wakati wa kilimo. Kuna majembe ya aina mbalimbali, mfano, jembe la mkono, jembe la kukokotwa na ng'ombe. Hali kadhalika, kuna majembe ya kufungwa na kukokotwa na trekta. Hii yote ni kumwezesha mkulima alime na kupata mazao ya kuridhisha ili aweze kujikimu.

Read More
Mwembe Wa Uwani Nyani Hatambi!

Mwembe Wa Uwani Nyani Hatambi!

Ni kawaida kwa jamii nyingi kupanda miti ya matunda uwani kwa nyumba zao. Miti ya matunda hii ni kama miparachichi, miembe, mikomamanga na kadhalika. Kwa kufanya hivyo, watu hawa wanakuwa na uhakika wa kupata mavuno na kuyafaidi kwa sababu ndege pamoja na wanyama waharibifu, kama nyani, ngedere nk hawawezi kutamba hapo kutokana na ukweli kwamba wakati wote kunakuwepo na watu. Endapo wanyama hao watakuja, lazima watafukuzwa na wenye matunda.

Read More
Angalia Namna Ya Kuongea Kwako.

Angalia Namna Ya Kuongea Kwako.

Lugha inaweza kubadilisha hali ya hewa katika mambo mengi ufanyayo. Matumizi ya lugha yanaweza kubadilisha maisha yako na jamii inayokuzunguka. Maisha ya ndoa yako, kama wewe ni mwanandoa, yanaweza kubadilika pia. Malezi ya watoto yanaweza yakabadilika katika familia zetu kutokana na luga tunazotumia. Lugha kali kwa watoto huwaogopesha kiasi hata kukosa amani na wazazi. Watoto wakiishi kwa woga, wanaweza hata kuingia kwenye makundi mabaya ili kupata faraja. Nyumbani watapaogopa, hawatapenda kukaa na hasa pale mzazi mwenye lugha ya kukera akiwepo. Watoto wakiishi katika mazingira hayo, wanaweza kujifunza mambo yasiyofaa. Wahenga walisema, samaki mkunje angali mbichi, akikauka hakunjiki.

Read More
Wema Sio Deni, Usisubiri Kulipwa.

Wema Sio Deni, Usisubiri Kulipwa.

Kuna tabia iliyojengeka katika jamii ya kufikiria kuwa unayemfanyia wema ni lazima akulipe. Kuna wale ambao wamesomesha watoto, ndugu na jamaa wengi tu kwa kutegemea kuwa watarudishiwa fadhila kwa wema walioufanya. Kwa bahati mbaya, watu hawa hungojea weee na kukuta hakuna majibu wala fadhila yoyote inayokuja. Hizo huwa ni hisia au mategemeo ya walio wengi.

Read More
Ujuzi Hauzeeki!

Ujuzi Hauzeeki!

Ujuzi ni ufundi au kipaji cha kufanya vitu ili kukuletea faida au kukuingizia kipato. Ujuzi unaweza kupatikana kupitia mafunzo. Hali kadhalika, ujuzi unaweza kutokana na kipaji cha kuzaliwa nacho mtu ambacho kinamuwezesha kufanya vitu vya pekee na vizuri vinavyoweza kununuliwa na watu na hivyo kukupatia kipato.

Read More
Haki Ya Mtu Hailiki!

Haki Ya Mtu Hailiki!

Haki ni kitu halali kinyume cha batili. Mwenye kutoa haki ni Mwenyezi Mungu peke yake, Yeye akisema amesema huwa hakuna wa kumpinga. Mwenyezi Mungu anaweza kuwatumia watu wakupatie haki yako. Mara nyingi tunaona na kuthibitisha ukweli wa usemi huu wa haki ya mtu hailiki bali hucheleweshwa tu.

Read More