
Maamuzi Yako Leo Ndiyo Mlango Wako Wa Kutokea Kesho!
Kimaisha, binadamu tunapitia pilikapilika mbalimbali. Nyingine ni za furaha na wakati mwingine ni za huzuni zenye kukatisha tamaa.

Unakimblia Wapi Unapopatwa Na Jambo?
Yako mambo yanayotokea katika maisha ya mtu pasipo yeye mwenyewe kujua. Mambo hayo yanaweza yakawa mazuri au mabaya lakini pengine yeye haelewi nini kinaendelea.

Utayari Una Faida.
Utayari maana yake ni kujitoa kufanya jambo lililokusudiwa na ndio ufunguo wa maisha. Ni ile shauku ya kutaka kufanya jambo na kuzingatia sawasawa na vile unavyoagizwa.Unapozingatia na kutii, ni lazima utakutana na usitawi wako katika kila jambo unalokusudia.

Njia Ya Muongo Ni Fupi!
Mlimbua nchi ni mtu ambaye anaifahamu sana nchi yake. Kwamaneno ya sasa huyu mlimbua nchi tunasema mhujumu wa nchi yaani anaisema vibaya nchi yake; anatoa siri za nchi yake, anaiweka nchi yake katika hali ya hatari kwa namna yeyote anayotaka yeye.

Tunda Jema Halikai Mtini.
Matunda ni aina ya chakula ambayo hulinda miili yetu na magonjwa mbalimbali. Katika mada hii, tunaongelea juu ya tunda ambalo ni moja kati ya matunda mengi yanayosifiwa kuwa ni mema na mazuri. Hii ni wazi tunda lolote lililo zuri haliwezi kukaa sana mtini maana lazima lichumwe mapema na kuliwa.

Jembe Halimtupi Mkulima!
Jembe ni nyenzo inayotumika na mkulima wakati wa kilimo. Kuna majembe ya aina mbalimbali, mfano, jembe la mkono, jembe la kukokotwa na ng'ombe. Hali kadhalika, kuna majembe ya kufungwa na kukokotwa na trekta. Hii yote ni kumwezesha mkulima alime na kupata mazao ya kuridhisha ili aweze kujikimu.

Mkia Ukatikapo Ng'ombe Huona Umuhimu Wake!
Mlimbua nchi ni mtu ambaye anaifahamu sana nchi yake. Kwamaneno ya sasa huyu mlimbua nchi tunasema mhujumu wa nchi yaani anaisema vibaya nchi yake; anatoa siri za nchi yake, anaiweka nchi yake katika hali ya hatari kwa namna yeyote anayotaka yeye.

Mwembe Wa Uwani Nyani Hatambi!
Ni kawaida kwa jamii nyingi kupanda miti ya matunda uwani kwa nyumba zao. Miti ya matunda hii ni kama miparachichi, miembe, mikomamanga na kadhalika. Kwa kufanya hivyo, watu hawa wanakuwa na uhakika wa kupata mavuno na kuyafaidi kwa sababu ndege pamoja na wanyama waharibifu, kama nyani, ngedere nk hawawezi kutamba hapo kutokana na ukweli kwamba wakati wote kunakuwepo na watu. Endapo wanyama hao watakuja, lazima watafukuzwa na wenye matunda.

Mwana Mtukutu Hali Ugali Mkavu!
Wazazi wengi tunabarikiwa na Mungu kupata watoto na ndio furaha kubwa katika ndoa zilizo nyingi. Hata hivyo, wapo wanandoa wengine ambao hawajabarikiwa kupata watoto. Yote ni kazi ya Mungu.

Raha Jipe Mwenyewe!
Furaha ni hali ya kuishi kwa amani na utulivu bila msongo wa mawazo. Msongo wa mawazo ni hali ya kuwa na stress mbalimbali zinazokusumbua katika maisha, kama vile huzuni, kukosa amani na raha, kuwa na mawazo mengi n.k.

Shujaa Haangamizwi Na Mwoga!
Shujaa ni yule mtu ambaye haogopi kuthubutu katika jambo lolote. Hata kama mahali ni pagumu, atajitahidi ili apite au atimize lengo alilokusudia. Mara nyingi mbele yake woga unakuwa haupo. Shujaa huwa anaangalia malengo yake kwa makini.

Angalia Namna Ya Kuongea Kwako.
Lugha inaweza kubadilisha hali ya hewa katika mambo mengi ufanyayo. Matumizi ya lugha yanaweza kubadilisha maisha yako na jamii inayokuzunguka. Maisha ya ndoa yako, kama wewe ni mwanandoa, yanaweza kubadilika pia. Malezi ya watoto yanaweza yakabadilika katika familia zetu kutokana na luga tunazotumia. Lugha kali kwa watoto huwaogopesha kiasi hata kukosa amani na wazazi. Watoto wakiishi kwa woga, wanaweza hata kuingia kwenye makundi mabaya ili kupata faraja. Nyumbani watapaogopa, hawatapenda kukaa na hasa pale mzazi mwenye lugha ya kukera akiwepo. Watoto wakiishi katika mazingira hayo, wanaweza kujifunza mambo yasiyofaa. Wahenga walisema, samaki mkunje angali mbichi, akikauka hakunjiki.

Heshimu Muda Nao Utakuheshimu.
Muda ni kitu cha thamani sana ambacho tumepewa bure na Mwenyenzi Mungu. Kila mtu amepewa bila upendeleo. Kwa kawaida, ukiuheshimu na kuujali muda, nao utakulipa kwani utaona matokeo tatakayokuja kuwa ni mazuri.

Wema Sio Deni, Usisubiri Kulipwa.
Kuna tabia iliyojengeka katika jamii ya kufikiria kuwa unayemfanyia wema ni lazima akulipe. Kuna wale ambao wamesomesha watoto, ndugu na jamaa wengi tu kwa kutegemea kuwa watarudishiwa fadhila kwa wema walioufanya. Kwa bahati mbaya, watu hawa hungojea weee na kukuta hakuna majibu wala fadhila yoyote inayokuja. Hizo huwa ni hisia au mategemeo ya walio wengi.

Mtaka Cha Uvunguni, Shart Ainame!
Hakuna mafanikio yatakayokujia ukiwa umekaa tu ma kubweteka huku ulingojea msaada kutoka kwa ndugu, jamaa na marafik. Mafanikio yanahitaji kujishughulisha ili uweze kuhimili changamoto zinazojitokeza. Maana kila unachokifikiria lazima kitakuwa na pingamizi au maswali ambayo ni hasi na magumu.

Tabia Zako Zinaweza Kukufanya Upoteze Fedha Zako!
Tabia zako zinaweza kukufanya upoteze fedha zako, ziwe nyingi au chache.

Ujuzi Hauzeeki!
Ujuzi ni ufundi au kipaji cha kufanya vitu ili kukuletea faida au kukuingizia kipato. Ujuzi unaweza kupatikana kupitia mafunzo. Hali kadhalika, ujuzi unaweza kutokana na kipaji cha kuzaliwa nacho mtu ambacho kinamuwezesha kufanya vitu vya pekee na vizuri vinavyoweza kununuliwa na watu na hivyo kukupatia kipato.

Mlibua Nchi Ni Mwananchi.
Mlimbua nchi ni mtu ambaye anaifahamu sana nchi yake. Kwamaneno ya sasa huyu mlimbua nchi tunasema mhujumu wa nchi yaani anaisema vibaya nchi yake; anatoa siri za nchi yake, anaiweka nchi yake katika hali ya hatari kwa namna yeyote anayotaka yeye.

Haki Ya Mtu Hailiki!
Haki ni kitu halali kinyume cha batili. Mwenye kutoa haki ni Mwenyezi Mungu peke yake, Yeye akisema amesema huwa hakuna wa kumpinga. Mwenyezi Mungu anaweza kuwatumia watu wakupatie haki yako. Mara nyingi tunaona na kuthibitisha ukweli wa usemi huu wa haki ya mtu hailiki bali hucheleweshwa tu.

Unaeokota Naye Kuni Ndiye Unaeota Naye Moto.
Kuni ni mojawapo ya nishati inayotumika sana barani Afrika. Kwa kawaida, kuni zinaokotwa au kukusanywa kutoka kwenye miti porini.