Mafanikio Ya Mtu Hutegemea Uwezo Wa Kufikiri Na Kutafakari
Mafanikio ya mtu yeyote hapa duniani hutokana na bidii, kujiamini, kiwango na uwezo wake wa kufikiri na kutafakari. Aidha, wengine hupoteza muda wao kuwaza jinsi watu wengine wanavyowaona, wanavyowafikiria, wanavyowatafakari na wanayowawazia.Hata hivyo inabidi kujua kwamba, ili uweze kufanikiwa katika maisha, kamwe usitumie muda wako kuwaza kuwa nikifanya hivi wengine watanionaje ama watanifikiriaje. Inakubidi wewe ufanye shughuli zako kwa kujiamini. Ili mradi unachofanya kiwe ni sahihi mbele ya Mungu na mbele za binadamu wenzio.Kwa kuwa na mtizamo huo chanya, mawazo ya watu wengine hayataruhusiwa kuitawala akili yako. Mtazamo chanya utakufanya usimame imara kwenye kile unachokiamini na hatimaye, utapata mafanikio.Hapa tunapata funzo kuwa, kamwe tusiumize vichwa vyetu na kuchukua muda mwingi kuwafikiria watu wengine wanachowaza juu yetu. Jiulize wewe unawaza nini kuhusu wao pamoja na kwamba hata wewe siyo kazi yako kuwawazia wengine. Wewe jali kazi na maisha yako na mambo yanayokuhusu. Acha kuwafikiria wao kwani mambo yao wewe hayakuhusu.
Asiye Uliza Hana Cha Kujifunza
Kuuliza ni tendo la kutaka kufahamu au kujua jambo ambalo hulijui au hulifahamu. Inawezekana pia hilo jambo unalifahamu lakini huna hakika kama hicho unachokifahamu ni sahihi. Kwa hiyo unatafuta kuelekezwa zaidi na mtu mwingine.
Siyo Kila Unalofanya Litampendeza Mwingine
Katika jamii inayotuzunguka siyo kila mtu ni mzuri kwako, laa hasha. Wabaya wapo wengi pia. Kuna watu ambao hawapendi mafanikio au maendeleo ya watu wengine. Mara nyingine unajikuta kwenye jamii ambayo kila wakati unapingwa na kudharauliwa. Kila utakachofanya unakosolewa bila sababu ya msingi. Binadamu kwa kweli ni kiumbe wa ajabu.
Zimwi Likujualo, Halikuli Likakwisha
Katika maisha, watu tunaishi kwa kufahamiana na kujuana. Kuelewana huko kuko katika tabaka mbalimbali, mathalani, kwenye jamii zetu, familia zetu na hata kwenye makundi maalumu. Hata kwenye sehemu za kazi matabaka haya ama makundi haya hujitokeza sana. Huwa kuna upendeleo dhahiri unaotokana na kufahamiana, hilali hiyo ipo.
Debe Tupu Haliachi Kutika
Tupo katika ulimwengu wenye mambo mengi yanayotuzuguka. Kwa kawaida, maisha yetu yako katika makundi makundi. Yapo makundi yenye uwezo mkubwa, yapo yale yenye uwezo wa kati, hali kadhalika yale ya kawaida. Kundi hili la mwisho ni lile ambalo inawezekana hata riziki ya siku ni ya kubabaisha. Inaweza hata siku ikapita bila ya kuwa na chochote.
Kumbuka Kuna Kesho
Unapoishi na watu hapa duniani, tambua kuwa kuna kesho. Aidha, unapokuwa kiongozi wa watu sehemu fulani kumbuka pia kuna kesho. Unapokuwa na madaraka, nafasi ya juu, kipato kizuri, na mwenye kutoa maamuzi ya juu, kumbuka kuna kesho.
Kua Makini, Chunguza Ushauri Unaopewa Kabla Ya Maamuzi
Ushauri ni maoni yanayotolewa kwa mtu ili yamsaidie kupata suluhisho kwenye changamoto anazopitia. Aidha, ushauri ni maelekezo ya kitaalamu yanayotolewa kwa mtu yeyote ili kumwezesha kufanya jambo fulani.
Hakuna Mtu Duniani Anayeweza Kuziba Pengo La Mtu Mwingine
Duniani kila mtu alikuja kwa wakati na majira yake. Hata mapacha waliigia duniani kwa muda tofauti. Kila mtu amekuja duniani kwa kusudi lililopangwa na Muumba wake. Katika hali hiyo hiyo basi, kila mtu ataondoka kwa wakati wake. Haijalishi kama mlizaliwa mapacha. Hii ina maana kuwa mmoja akiondoka, linabaki pengo lisilozibika.
Jifunze Kujishusha Machoni Pa Watu Wengine
Baadhi ya watu wana ile tabia ya kuona kwamba wao ndio pekee wa kuweza kutoa maamuzi ya aina yoyote wakiwa kwenye kundi la watu. Tabia ya watu hawa ni ya kujiona na kujisikia kuwa wao ni bora kuliko watu wengine. Watu hawa hufikia hatua ya kuchukia pale wanapotoa jambo/ushauri mbele za watu na halafu usikubaliwe. Huwa hawaelewi kabisa kwa nini yale wanayosema yasikubaliwe na watu.
Ujana ni Dhahabu
Katika maisha tunaweza kusema kuwa, "umri wa ujana" ni kipindi cha dhahabu ambacho tunatengeneza marafiki wengi na kupoteza wengi pia. Katika kipindi hiki, uamuzi wa kuyaharibu au kuyatengeneza maisha yako ili yawe mazuri baadaye unao wewe mwenyewe. Kwa hiyo inakupasa kukumbuka kuwa kipindi hiki kikishapita hakijirudii tena. Hivyo kitumie vizuri uwezavyo.
Usitoe Maamuzi Wakati Una Hasira
Hasira ni ile hali ya kuhamaki kwa jambo ambalo umesikia au umefanyiwa na mtu bila kukubaliana ama kuridhika nalo. Inawezekana likawa ni jambo la kusingiziwa au la. Hasira inaweza kukupelekea kuamua chochote kibaya, ukafikia hata hatua ya kuua. Mara nyingi hasira inaishia kwenye kujuta kwa lile ulilolifanya kwa kukusudia ama kutokusudia. Sambamba na usemi huu ni ule wa Majuto ni Mjukuu. Tunaaswa kutokuamua jambo lolote wakati tuna hasira.
Heri Nitakula na Nani Kuliko Nitakula Nini
Maisha tuishio yapo katika matabaka tofauti. Wapo watu wenye uwezo sana, wapo wale wenye uwezo wa kati na wale wenye uwezo wa chini. Ni muhimu kujua kuwa maisha yetu sisi binadamu yanatofautiana.
Ukipanda Cheo Usisahau Familia Yako
Cheo ni aina mojawapo ya usitawi au baraka azipatazo mwanadamu katika mazingira yake ya kazi. Hata mfanya biashara anapokuwa amekua kibiashara, nako pia ni kama kupanda cheo.
Kinga ni Bora Kuliko Tiba
Kinga ni kudhibiti tukio au jambo kabla halijaleta madhara. Tukio linaweza kuwa ni ugonjwa au mambo mengine yawayo.
Tunza Siri za Kazi Zako kwa Mafanikio Yako
Hapa duniani kuna baadhi ya watu wenye makelele na fujo nyingi ambao hujigamba bila hata kuulizwa maswali yanayohusu kazi wazifanyazo.
Maisha ni Mafupi, Tusiache Kutenda Mema
Kutenda mema au wema ni silaha kubwa katika maisha yetu. Kuishi hapa duniani ni kwa neema tu ambayo mtu hujaliwa na Muumba wetu. Hatuna uhakika na siku zetu za hapa duniani. Hatuna uhakika kama tutamaliza salama siku zetu zilizosalia ama laa, hiyo ni siri ya Mwenyezi Mungu pekee.
Mvuvi Ajua Pweza Alipo
Mvuvi ni mtu anayevua samaki kwa ajili ya biashara. Akifanikiwa kupata samaki wengi, wengine huwaacha kwa ajili ya matumizi ya nyumbani. Hiyo ndio kawaida ya wavuvi. Pweza ni samaki anayependwa sana na watu hasa watu waisio ukanda wa pwani. Pweza huwa wanauzwa kwa bei mbaya sana.
Maji Yanayokimbia Huyapitia Maji Yaliyosimama
Maji yanayokimbia mara nyingi ni maji ya kwenye mto. Na kuna yale maji yoliyotuama au kusimama yapo kando ambayo yawezekana yamekwamishwa na majani au kuzidiwa na udongo.
Nyakati Ngumu Ndio Thibitisho la Ujasiri Wako
Nyakati ngumu ni kipindi ambacho kila mtu hupitia katika maisha yake. Katika kipindi hicho, inawezekana hali ya uchumi ikawa imeyumba na kuyafanya mambo yasiende ipasavyo. Kama una ujasiri, hali hiyo haitakuchanganya bali utaendelea kuwa na amani. Lakini usipokuwa jasiri, kila mtu ataelewa kuwa unapitia kwenye hali ngumu, hiyo haitakuwa sahihi hata kidogo.
Mpende Adui Yako
Adui ni mtu ambaye huna mahusiano mazuri naye. Mtu huyu utamtambua kuwa ni adui kwa matendo yake na hata kuongea kwake. Mara nyingi adui yako kila atakaloongea kwako huwa ni hasi na pia huwa halina amani.