Mgeni Njoo, Mwenyeji Apone

Mgeni Njoo, Mwenyeji Apone

Mgeni ni mtu anayekuja kwenye makazi ambayo hana mazoea nayo au ni mahali ambapo siyo kwake. Kwa kawaida, mtu huyu anapokuja humfanya mwenyeji wake kuhangaika kutafuta hiki na kile, ili mradi yeye na mgeni wake waweze kufurahi pamoja. Mgeni huyo anaweza kuwa ni ndugu ambaye ametoka mbali kuja kusalimia tu ama kwa shughuli nyingine.

Read More
Ni Rahisi Kubeba Kikombe Kisicho na Kitu Kuliko Kile Chenye Kitu

Ni Rahisi Kubeba Kikombe Kisicho na Kitu Kuliko Kile Chenye Kitu

Kwenye maisha ya binadamu, tunaposema “Ni rahisi kubeba kikombe kisicho na kitu kuliko kikombe chenye kitu“, ina maana kubwa. Kwa mfano, ukiishi na watu mbalimbali huku ukijivuna, ukiwadharau na kuwaona hawafai, hawajui kitu, ila wewe unajihesabia kuwa ndiye unayejua kila kitu, watu watakulinganisha au watakufananisha na kikombe kisicho na kitu chochote ndani yake, yaani kikombe kitupu.

Read More
Jifunze Kutotangaza Shida Zako

Jifunze Kutotangaza Shida Zako

Tatizo au shida humpata mwanadamu yeyote hapa duniani. Huo ndio ukweli wa maisha, kwani maisha ndivyo yalivyo. Kawaida, mtu akipata tatizo, hali yake hubadilika na tunaweza tukasema kuwa, mtu huyo huwa hayuko sawa. Anaweza akatafuta namna ya kutoka au kulitatua jambo linalomsibu. Kufanya hivyo ni hali ya kawaida sana.

Read More
Kikulacho Ki Nguoni Mwako

Kikulacho Ki Nguoni Mwako

Neno kikulacho linaelezea uharibifu ambao unaweza kutokea au kufanyika kwa makusudi au bila kukusudia ili kumuharibia mtu. Mara nyingi hilo jambo hutokea kwa watu wanaoelewana vizuri. Zaidi ni marafiki ambao huwa wanafanyiana hivyo. Hii ni kwa sababu kila mmoja anamuelewa mwenzake vizuri. Inawezekana akawa ni jirani yako au ndugu yako.

Read More
Ulimi Ulimponza Kichwa

Ulimi Ulimponza Kichwa

Ulimi ni kiungo kidogo ndani ya mwili, hukaa mdomoni na kumwezesha mtu kuongea vizuri. Kama ulimi haufanyi kazi basi mtu hawezi kuongea vizuri na mara nyingi huwa bubu.

Read More
Shida Haipigi Hodi

Shida Haipigi Hodi

Shida ni tatizo au changamoto inayomfika mwanadamu. Hodi ni neno linalotumika badala ya swali la: “naweza kuingia?" Hapa anaposema shida haina hodi sio kweli maana mwanadamu anapopatwa na tatizo ataingia kwa jirani na kutoa shida zake ikibidi kuomba msaada ili atatue changamoto zake. Shida inaweza kukupeleka hata mahali ambapo hujawahi kufika.

Read More
Mbuzi Hula Kadiri Ya Urefu Wa Kamba Yake

Mbuzi Hula Kadiri Ya Urefu Wa Kamba Yake

Mbuzi ni mnyama anayefugwa kama wanyama wengine. Akipelekwa machungani huwa anafungwa kamba mguuni ili kumuwekea mipaka ya malisho yake. Mara nyingi akiachiwa huru au akikata kamba anaenda kufanya uharibifu kwa kula kwenye mashamba ya watu na mwenye mbuzi hupata kesi kubwa. Mara nyingine huweza hata kulipishwa kwa uharibifu huo uliosababishwa na mbuzi wake. Hii ndio sababu kuu ya kufungwa kwa kamba.

Read More