Cha Ndugu Hakiwezi Kua Chako, Kiogope

Cha Ndugu Hakiwezi Kua Chako, Kiogope

Watu wengi hupenda sana kujisifu kutokana na kile alicho nacho ndugu yake. Ni ukweli usiopingika kuwa mtu yeyote hatakiwi kujisifu kwa ajili ya mali ya ndugu yake. Hii ni kutokana na ukweli kuwa vitu hivyo au mali hizo siyo za kwake. Kila mtu yampasa atafute kilicho chake. Kitu kikiwa cha kwako unakuwa na uhuru nacho na unaweza ukafanya nacho chochote unachotaka.

Read More
Chui Hakumbatiwi

Chui Hakumbatiwi

Fikira za mwanadamu huwa hazina ukomo. Hii ni kutokana na ukweli kwamba binadamu ana mambo mengi ya kuwaza wakati wote. Kuna mambo tunayawaza yakiwa ni ya hatari kwetu na ya kuhuzunisha pia. Mambo ya kuhuzunisha huwezi kuyakumbatia. Mambo hayo ni kama uvivu, wizi, kutowajibika, kusengenya na kusema uongo. Ukitaka kuwa na amani, inakupasa ujitenge na mambo hayo, hii ni kwa ajili ya ustawi wako mwenyewe.

Read More
Jipe Muda Wa Kufurahia Yale Uliyobarikiwa

Jipe Muda Wa Kufurahia Yale Uliyobarikiwa

Ni jambo la kawaida kabisa kwa binadamu kupenda kuwa na furaha siku zote za maisha yake. Lakini yatupasa tuelewe kuwa furaha hiyo haipatikani ki urahisi. Inakupasa kuhangaika na kujishugulisha ili uweze kutimiza matakwa yako na ufurahie matunda ya kazi zako. Lakini badala ya kujishughulisha, inafikia wakati tunaangalia fulani kafanya hiki au kile na ndio maana kafanikiwa zaidi. Tunafikiria kuwa mafanikio yake huenda yalipatikana kiurahisi. Hatuchukui muda kuchunguza alikotoka hadi akafikia hapo alipo. Tunafikiri yote aliyonayo aliyapata kiurahisi tu.

Read More